Diamond kuuza nyimbo mtandaoni

 

NA HUMPHREY SHAO, DAR ES SALAAM
MSANII wa muziki wa Bongo Fleva, Nasib Abdul ‘Diamond’, jana aliingia makubaliano na mtandao wa Muziki Family, ambao utakuwa ukitangaza nyimbo zake kwa njia ya mtandao.
Akizungumza jijini jana, Mkurugenzi mtendani wa kampuni ya Spice Vas Afrika, ambao ndiyo wamiliki wa mtandao huo, Arun Nagar, alisema makubaliano hayo yatamuongezea mashabiki wengi msanii huyo.
 
kwanza Tanzania kuingia mkataba na Alisema kuwa Diamond ni msanii wa kampuni hiyo ambayo ina jumla ya wasanii 100 wa kimataifa.
“Tutashirikiana kwa kila kitu kuhakikisha muziki wa Diamond unafanya vizuri Afrika, huku mashabiki wakiongezeka upande wake na wetu pia,” alisema Nagar.

Wakati huo huo, Diamond alisema kuwa anashukuru kuingia makubaliano hayo yatawawezesha mashabiki zake kusikiliza nyimbo zake kupitia mtandaoni Afrika.

Post a Comment

Previous Post Next Post