NA HUMPHREY SHAO, DAR ES SALAAM
MSANII wa muziki wa Bongo Fleva, Nasib Abdul ‘Diamond’,
jana aliingia makubaliano na mtandao wa Muziki Family, ambao utakuwa ukitangaza
nyimbo zake kwa njia ya mtandao.
Akizungumza jijini jana, Mkurugenzi mtendani wa
kampuni ya Spice Vas Afrika, ambao ndiyo wamiliki wa mtandao huo, Arun Nagar,
alisema makubaliano hayo yatamuongezea mashabiki wengi msanii huyo.
kwanza Tanzania kuingia mkataba na Alisema kuwa
Diamond ni msanii wa kampuni hiyo ambayo ina jumla ya wasanii 100 wa kimataifa.
“Tutashirikiana kwa kila kitu kuhakikisha muziki wa
Diamond unafanya vizuri Afrika, huku mashabiki wakiongezeka upande wake na wetu
pia,” alisema Nagar.
Wakati huo huo, Diamond alisema kuwa anashukuru
kuingia makubaliano hayo yatawawezesha mashabiki zake kusikiliza nyimbo zake
kupitia mtandaoni Afrika.