TANZANIA ALBINO UNITY WAPATA MAFUNZO YA UFUGAJI KUKU


Tanzania Albino Unity ni kikundi cha walemavu wa Ngozi (Albino) kilichoanzishwa mwaka 2013 chenye lengo na madhumuni ya kupunguza makali ya maisha na mazingira magumu ambayo watu wenye ulemavu wanakumbana nayo.Taasisi hii iliyoanzishwa.inayoongozwa na inayosimaiwa na watu wenye ulemavu imesajii brela chini ya majina ya kampuni.kwa usajili namba 275829 Kwa sasa Asasi imeamua kujikita katika eneo la ufugaji wa kuku wa nyama kama njia ya kuongeza ajira binafsi kwa watu wenye ulemavu ikianzia Manispaa ya Temeke na tunategemea kutafuta ufumuzi wa changamoto za ajira kwa albino katika wilaya na mikoa mingine ya Tanzania.

Tanzania Albino Unity kwa uwezeshaji kutoka, Tume ya uwezeshaji imepata nafasi ya kuwakilisha Maalbino 6 kushiriki mafunzo ya siku 14 ya ufugaji wa kuku wa nyama katika chuo cha wakala wa vyuo vya mifugo kilichopo Vetenari, Temeke, Dar-es-salaam.Malengo ya mafunzo mafunzo haya ni kuwezesha maalbino kuwa na uelewa na mbinu za kufanya ufugaji bora na wa kisasa wa kuku wa nyama ili waweze kuendesha mradi wa ufugaji na kukuza kipato chao.

Taarifa hii inatoa kwa muhutasari mchakato wa mafunzo haya toka siku ya kwanza mpaka siku ya mwisho wa mafunzo.

1.0 MCHAKATO WA MAFUNZO
Mafunzo ya ufugaji wa kuku yalichukua muda wa siku 14 yakihusisha mafunzo ya darasani na mafunzo kwa vitendo ili kuwezesha walengwa kuelewa kwa undani hatua mbalimbali za ufugaji wa kuku.

      2.1 MUDA WA MFUNZO NA IDADI YA WALENGWA
Muda wa mafunzo ulikuwa ni siku 14 na idadi ya walengwa ilikuwa ni Maalbino 6

         2.2 MAFUNZO TULIYOJIFUNZA
Katika muda wa siku 14 tuliweza kupitia maeneo mbalimbali muhimu katika ufugaji wa kuku ambazo tunazieleza kwa muhutasari hapo chini kutokana na utaratibu na ratiba iliyopangwa na wakufunzi:-

             2.2.1 Utunzaji bora wa kuku
Hapa tulifunza dhana nzima ya utunzaji wa kuku yakuwa kuku ni kama ndege ambaye anafugwa nyumbani ambao wanagawanywa katika makundi makuu 2.Ambao ni kuku wa kienyeji na kuku wa kisasa.Na kuwa kuku wa kisasa pia wamegawanyika katika sehemu 2 ambazo ni kuku wa nyama na kuku wa mayai.Kuku hawa wa kisasa wanatakiwa kufugwa kwa taratibu za kitaalam ikiwa ni pamoja na ujenzi wa banda linalokidhi mahitaji ya kuku hao.

             2.2.2 Magonjwa ya kuku
Pamoja na utunzaji bora wa kuku tulijifunza magonjwa yayodhoofisha ukuaji wa kuku pamoja na kusababisha vifo kwa kuku kuwa ni:-
-Mdondo/kideri unaonekana katika mifumo ya hewafahamu, chakula na mfumo wa uzazi ugonjwa huu unaweza kuua kuku kwa 80% mpaka 100% katika banda.
-Respiratory disease complex –Ugonjwa huu wa mfumo wa hewa unaweza kuua kuku katika banda kwa 5 hadi 10%

-Mafua ya kuku-hugonjwa huu huweza kuambukiza kuku wengine kwa haraka katika banda kiwango cha vifo vya kuku huwez kufikia 20% na huambukizwa kwa njia ya jicho au pua.
-Ugonjwa wa viungo vya ndani-njia za maambukizi za ugonjwa huu ni kwa njia ya chakula na kiwango cha vifo vya kuku huwa ni kwa 5-20%
-Gumbolo-ugonjwa uliogunduliwa kwa mara ya kwanza 1962.uwezekano wa kuambukizana ni kubwa sana.Kiwango cha vifo kinaweza kuwa kwa 20%-60%
-Ugonjwa wa kuharisha njano-huua kuku kwa 70-80% bandani
Lakini pamoja na kujifunza magonjwa tumejifunza dalili,njia za kwalinda kuku dhidi ya magonjwahayo kwa kutumia chanjo mbalimbali za magonjwa hayo.

             2.2.3 Lishe ya kuku
Pamoja na kujifunza lishe za kuku wa nyama tulianza na vifaa vya kulishia kuku ambavyo ni pamoja na vifaa vya kulia chakula(feeder),vifaa vya kunywea maji(drinker) na chanzo cha joto kama vile umeme,jiko la mkaa,taa ya mafuta.

     


Kushoto pichani: Buruda la kukuzia vifaranga linavyoonekana likiwa na miundo mbinu ya umeme chakula na maji, buruda hili lilitumika katika mafunzo ya vitend.Kulia ni walengwa wamafunzo wakiwa katika mafunzo ya vitendo. 

                    Lishe ni pamoja na:-
Chakula cha kuanzia, hupewa kuku wa kuanzia umri wa siku 1-siku 21(wiki ya 1 hadi 3)
Growers, Chakula hiki hupewa kuku kuanzia umri wa siku 22 –siku 28
Chakula cha kumaliziachakula hiki huanzishwa mwishoni mwa wiki ya tatu na huwa kinachanganywa na starter kwa muda wa siku 3-4 kabla ya kuacha kabisa kuwapa starter.
Maji –kuku wa nyama huitaji maji safi na salama wakati wote yanayowekwa katika vyombo visafi, salama na vinavyowezesha kuku kunywa maji kwa usalama.
Pia tumejifunza kuhusu utunzaji wa chakula cha kuku.

             2.2.4 Utunzaji wa kumbukumbu
Katika utunzaji wa kuku tumejifunza kuweka kumbukumbu ya matukioa kadhaa muhimu katika ufugaji wa kuku, kama vile:-
·   Kumbukumbu za mfugaji mwenyewe
·   Taarifa kuhusu kuku wenyewe toka kuwasili
·   Kumbuumbu za vifo
·   Kumbukumbu ya manunuz ya chakula
·   Kumbukumbu ya tiba na chanjo
·   Kumbukumbu Matumizi ya maji
·   Kumbukumbu Huduma mbalimbali
·   Kumbukumbu Mauzo y kuku

             2.2.5 Mafunzo kwa vitendo
Baada ya kujifunza kwa nadharia tulipata nafasi ya kujifunza ufugaji wa kuku kwa vitendo tukianzia na kuku 100.Mambo muhimu tuliyojifunza ni pamoja na:-

-Kundaa banda kabla ya kuweka vifaranga
-Kutenegeneza mahala pa kulelea vifaranga (buruda)
-Kupokea vifaranga
-Kutengeneza miundombinu ya joto
-Kulisha vifaranga na
-Kuchanja vifaranga

  3.0 MAFANIKIO
Ø Kuongezeka kwa uelewa wa walengwa (maalbino) 6 walioshiriki katika mafunzo kwa muda wa siku 14.
Ø Washiriki walishiriki kwa siku zote 14, hakukuwa na mgonjwa wala utoro.
Ø Tumejenga husiano mwema na wakufunzi na mafunzo na kuwa pamoja kwa hali wakati na baada ya mafunzo.

4.0 MAPENDEKEZO
4.1 Mapendekezo ya walengwa wa mafunzo.
ü  Washiriki wanashukuru kwa hatua muhimu katika mradi lakini wanapendekeza kuwa ufadhili uendelee ili kuwezesha mradi huu kutekelezwa mpaka mwisho.
ü  Wadu zaidi wajitikeze ili kuwezesha mafunzo haya kuwakifikia walengwa zaidi hata kama italazimika kutumia walengwa 6 waliowezeshwa kipindi hiki.
4.2 Mapendekezo ya wakufunzi
ü  Wakufunzi walipendekeza kuomba fedha ili kulipia mabanda ya chuo kwaajili ya shughuli za mradi wa ufugaji.
ü  Kuendelea kupeleka wanachama wa Albino unity na maalbino wengine ili kuwezesha mafunzo zaidi kwa albino.

5.0 HITIMISHO
Tanzania Albino Unity kwa uwezeshaji kutoka, Tume ya uwezeshaji imepata nafasi ya kuwakilisha Maalbino 6 kushiriki mafunzo ya siku 14 ya ufugaji wa kuku wa nyama katika chuo cha wakala wa vyuo vya mifugo kilichopo Vetenari, Temeke, Dar-es-salaam.

Wawakilishi hawa kwa uchache wake, tumedhamilia kuhakikisha kuwa tunajitahidi kwa kadili itakavyowezekana kuweka mafunzo tuliyopata katika vitendo.Tunamatarajio ya pamoja na kuyatuia kwaajili ya kwetu binafsi katika mradi, tutawasambazia Maalbino wengine ili kusambaza manufaa ya mafunzo haya.

Rai yetu ni kwa wadau mbalimbali kuunga mono juhudi za Tume za kutoa ufadhili ili kuwezesha utekelezaji wa mradi wote,kwa kuwa mafunzo ni sehemu tu ya mradi mzima wa ufugaji wa kuku wa nyama.Mradi huu ukifanyika utawezesha kuinua kipato cha Maalbino na hivy kupunguza hadha ya kuombaomba. Tunawasilisha.





Post a Comment

Previous Post Next Post