FINCA Tanzania imezindua ‘Fika na FINCA’, kampeni inayolenga
kuwafikia Watanzania wote kupitia huduma za kibenki na kuwasaidia kutimiza
malengo ya kimaendeleo waliyojiwekea. Mnamo Januari 2013 FINCA ilikuwa
microfinance ya kwanza kupata leseni kutoka Benki Kuu ya Tanzania inayoiruhusu
kupokea na kutunza akiba, na tangu hapo, mbali na mikopo ya aina mbalimbali,
FINCA imekuwa ikitoa huduma ya akaunti za akiba kwa wateja wake.
Faida za akaunti za akiba za FINCA ni nyingi, ikiwa ni
pamoja na urahisi wa kufungua na kuendesha akaunti, taratibu za kufungua
akaunti zina mahitaji madogo, kutoa na kuweka pesa ni bure kwenye matawi yote
nchini, na usalama wa fedha za mteja kupitia mfumo wa bayometriki unaotumiwa na
benki hiyo. Vilevile kupitia akaunti ya muda maalum (Mipango), FINCA inampatia
mteja faida kubwa zaidi ya 14%.
Mteja wa mara ya kwanza sasa anaweza kupata mkopo wa hadi
Tshs. milioni 150 ndani ya siku 5 tu. FINCA inatoa pia Mkopo wa Kilimo kwa
wakulima hasa wale walio katika maeneo ya vijijini na Mkopo wa Elimu kusaidia
wamiliki wa taasisi za elimu na wale wanaohitaji kulipia ada za watoto na ndugu
zao.
Kupitia njia mbalimbali za kutoa huduma, FINCA inaendelea
kurahisisha maisha ya mteja na kutoa kipaumbele kwa mahitaji ya mteja. Kwa
kutumia huduma za kibenki kupitia simu za mkononi na huduma ya wakala wa FINCA
Express iliyoanzishwa hivi karibuni, wateja wanaweza kupata huduma wakati
wowote, popote walipo.
Kwa zaidi ya miaka 16 FINCA imeaminiwa na wananchi katika
kuwapatia huduma za kifedha na inapanga kuendeleza viwango vyake kama benki
inayowajibika kuhudumia na kuwawezesha Watanzania kwa ujumla.
Kuhusu FINCA Tanzania:
FINCA Tanzania ni moja kati ya taasisi 23 za FINCA
Microfinance Holding Company (FMH), yenye makao yake makuu Washington DC nchini
Marekani na kuendesha shughuli zake katika bara za Latin America, Eurasia,
Mashariki ya Kati, na Afrika. FMH inahudumia karibu wateja 2,000,000. Wanahisa
wa FINCA ni pamoja na The International Finance Corporation (IFC) – ambayo ni
sehemu ya World Bank, The German Development Bank - KfW, The Dutch Development
Bank - FMO, ResponsAbility (kampuni ya Uwisi inayowajibika katika jamii kwenye
uwekezaji), TripleJump (kampuni ya Uholanzi inayowajibika katika jamii kwenye
uwekezaji), Nederlandse Financierings- Maatschappij voor Ontwikkelingslanden,
Credit Suisse Microfinance Fund Management Company, ASB-Novib
Microkredietfonds, FINCA International Inc.