sehemu ya uwanja wa uhuru ambao upo kwenye matengenezo
Hivyo, TFF inaelekeza nguvu zote katika kuandaa Fainali za Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka U17 mwaka 2019.
TFF inaamini kwa dhati kuwa uenyeji wa Afrika U17 2019 utaifungulia Tanzania milango ya kuandaa mashindano makubwa zaidi.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
limefahamishwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kuwa Tanzania haitaweza
kuwa mwenyeji wa Fainali za Afrika- AFCON 2017 kwa kuwa haijawahi kuandaa
fainali zozote za vijana Afrika. Fainali hizo ni zile za vijana wenye umri
chini ya miaka 17 na 20.
Hivyo, TFF inaelekeza nguvu zote katika kuandaa Fainali za Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka U17 mwaka 2019.
Tunapenda kuchukua fursa hii kumshukuru Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanazania, Jakaya Kikwete kwa kututia moyo katika kuomba
uenyeji wa AFCON 2017.
Pia tunamshukuru Waziri wa Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara kwa juhudi binafsi alizozionyesha katika
jitihada za Tanzania kuomba uenyeji wa AFCON
2017.
TFF inaamini kwa dhati kuwa uenyeji wa Afrika U17 2019 utaifungulia Tanzania milango ya kuandaa mashindano makubwa zaidi.
WANYARWANDA
KUCHEZESHA MECHI YA STARS
Waamuzi
kutoka Rwanda ndiyo watakaochezesha mechi ya Kalenda ya Shirikisho la Kimataifa
la Mpira wa Miguu (FIFA) kati ya Taifa Stars na Benin itakayofanyika Jumapili (Oktoba
12 mwaka huu) jijini Dar es Salaam.
Hakizimana
Louis ndiye atakayeongoza waamuzi hao wa FIFA kwa kupuliza filimbi kwenye mechi
hiyo itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 11 jioni.
Atasaidiwa na Simba Honore na Niyitegeka Jean Bosco.
Mechi
hiyo itatanguliwa na ile ya viongozi wa dini- Kiislamu vs Kikristo kudumumisha
upendo, amani na ushirikiano itakayoanza saa 9 kamili alasiri. Tiketi za
elektroniki zitakazotumika kwa mechi hiyo tayari zimeanza kuuzwa kwa kiingilio
cha sh. 4,000 na sh. 10,000.
Wakati
huo huo, Kocha Mart Nooij ameongeza wachezaji watatu kwenye kikosi cha Taifa
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ili kukiongezea nguvu kwa
ajili ya mechi hiyo.
Wachezaji
walioongezwa ni Jonas Mkude na Joram Mgeveke kutoka timu ya Simba, na Gadiel
Michael wa Azam.