Pindi chana asema serikali itapigania haki za watoto

 Eric Baume, head of cooperation to European Union,Tanzania



Na Humphrey Shao , Dar es Salaam
SERIKALI imetangaza kuendelea kudhibiti baadhi ya watu wasio waadilifu ambao wamekuwa na tabia ya kusafirisha watoto ndani na nje ya nchi kwa ajili ya kwenda kuwatumikisha kazi za majumbani.

Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Pindi Chana kwenye mkutano wa kujadili miaka 25 ya mkataba wa Haki za Watoto  Duniani.


Alisema ili kudhibitisha hilo katiba mpya inayotarajiwa kupigiwa kura ya maoni ya kuikubali au kuitakaa kuna ibara ya 53 inayozungumzia haki ya watoto ikiwamo ya kupata elimu, kupinga ukatili na kupata huduma za afya.



 Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Pindi Chana kwenye mkutano wa kujadili miaka 25 ya mkataba wa Haki za Watoto  Duniani.


“Serikali iliungana na mataifa mbalimbali Duniani ili kuridhia haki ya mtoto kulindwa, kupata elimu, afya na kuondoa ukatili wa jinsia.

“Ili kutekeleza hilo, katiba mpya ibara ya 53 inazungumzia haki ya watoto kwa ujumla, hivyo basi mtu atakayebainika anakwenda kinyume na haki hizo serikali itamchukulia hatua za kisheria,”alisema Chana.
Aliongeza kutokana na hali hiyo serikali imejipanga kuhakikisha kuwa inazuia biashara haramu ya watoto  pamoja na kudhibiti vitendo vya ukatili vinavyofanywa na baadhi ya watu ambao wamekuwa wakisafirisha binadamu wenzao kama wanyama katika nchi za Magharibi.
“ mkakati wa serikali ni kuhakikisha kuwa inashirikiana na wadau mbalimbali ili kufanikisha mipango na kuhakikisha kuwa haki ya mtoto inalindwa kuanzia nyumbani hadi katika jamii hili kupata kizazi ambacho kitakuwa na uadilifu na weredi”.

Post a Comment

Previous Post Next Post