Na Humphrey Shao, Dar es Salaam
KIPA wa
Yanga, Ally Mustapher ‘Barthez’ amewaomba radhi mashabiki, wapenzi na viongozi
wa timu hiyo kutokana na kipigo cha bao 1-0 walichokipata Jumapili kwenye
Uwanja wa Taifa dhidi ya mahasimu wao Simba.
mara baada ya mchezo huo Barthez alisema hakutarajia kupata matokeo
hayo na kitendo cha kutangulia kufungwa kulionekana kuwaondoa mchezoni karibu
wachezaji wote na kuanza kucheza kwa kukamiana.
“Binafasi
nawaomba radhi mashabiki, viongozi na wapenzi wa Yanga kwa kufungwa bao hilo
kwani hayakuwa matarajio yetu kupoteza mchezo ukizingatia kwa sasa tupo katika
kiwango kizuri hivyo kila mmoja alikuja uwanjani akitarajia kuona tunawafunga
watani zetu lakini hali imekuwa tofauti, alisema Barthe huku akitokwa na
machozi.
Katika
mchezo wa Jumapili Simba iliendeleza ubabe kwa mahasimu wao Yanga ambao ndiyo
vinara wa Ligi Kuu Tanzania bara wakiwa wamecheza michezo 16 huku wakiwa na
mchezo mmoja mkononi na wana pointi 31 wakifuatiwa na mabingwa watetezi Azam FC
wenye pointi 30.