KATIBU wa Halmashauri Kuu ya CCM
(NEC), Itikadi na Uenezi Nape Nnauye amempongeza Waziri Mkuu wa zamani na
Mbunge wa
Monduli Edward Lowassa kwa kukubali kuyasitisha makundi ya Watanzania wanaokwenda nyumbani kwake kumshawishi agombee
urais Oktoba 31, mwaka huu.
Monduli Edward Lowassa kwa kukubali kuyasitisha makundi ya Watanzania wanaokwenda nyumbani kwake kumshawishi agombee
urais Oktoba 31, mwaka huu.
Lowassa anayetajwa kugombea urais
mwaka huu amekuwa akipokea makundi tofauti ya wananchi nyumbani kwake Dodoma
yanayokwnda kumshawishi atangaze nia pindi muda utakapowadia.
Juzi Lowassa akipokea kundi jongine
LA vijana waendesha pikipiki bodaboda kutoka wilayani Mbarari mkoan
Mbeya fananisha makundi yanayokwenda kumshawishi sawa na mafuriko
hivyo hawezi kuyazuia kwa mkono.
Akizungumzia uamuzi huo wa Lowassa
wa kusitisha kuyapokea makundi hayo wilayani hapa Nape alimpongeza kwa kukubali
kutii maagizo ya Chama pamoja na kanuni zinazokiongoza Chama hicho.
"Nampongeza Lowassa kwa
kukubali kuheshimu kanuni, taratibu na Katiba ya chama ambayo ndio inatakiwa
kufuatwa na kila mmoja ndani ya chama.
"Alichokuwa anafanya lowassa ni
kufanya kuanza kampeni kabla ya wakati
na kwa mujibu wa chama chetu ni makosa maana anakiuka taratibu na
kanuni za chama.Hatuwezi kukaa kimya wakati kanuni zinavunjwa.hivyo
nimpongeze lowassa kwa kutii agizo la chama,"alisema nape.
na kwa mujibu wa chama chetu ni makosa maana anakiuka taratibu na
kanuni za chama.Hatuwezi kukaa kimya wakati kanuni zinavunjwa.hivyo
nimpongeze lowassa kwa kutii agizo la chama,"alisema nape.
Akizungumzia kuhusu wapambe wa
makada wa wanaotaka urais, aliwataka makada wote wanataka kugombea urais
kupitia chama hicho wawe makini na
wapambe wao.
wapambe wao.
Nape alifafanua kuwa ni vyema makada
wanaotaka kugombea urais wakawa makini na ushauri unaotolewa na washauri au
wapambe wao kwani unaweza kuwasababisha kupoteza sifa ndani ya CCM.
"Nawashauri wote wanaotaka
kugombea urais wasiwasikilize wapambe
kwani ushauri mwingine unaweza
kuwakosesha sifa za kugombea nafasi ya urais,"alisema Nape na kuongeza:
kwani ushauri mwingine unaweza
kuwakosesha sifa za kugombea nafasi ya urais,"alisema Nape na kuongeza:
"Na hili si kwa wapambe wa
Lowassa tu, bali ni kwa wapambe wa makada wore ndani ya CCM,"alisema.
Akisisitiza kuhusu CCM kutenda haki
Nape alisema kwamba Chama hicho kitahakikisha kinatenda haki kwa kila
anayeomba nafasi na hakuna ambaye
atanyimwa haki yake.
atanyimwa haki yake.
Alisema kwa wote ambao watakuwa
makini katika kuzingatia kanuni na
taratibu za chama haki zao zitalindwa lakini wale ambao watakiuka kwa
maksudi hao hatua za kinidhamu zitachukuliwa dhidi yao.
taratibu za chama haki zao zitalindwa lakini wale ambao watakiuka kwa
maksudi hao hatua za kinidhamu zitachukuliwa dhidi yao.
"Tunaendelea kuwakumbusha
makada wote kuzingatia kanuni na
Katiba ya chama.Kinyume cha hapo watakuwa wanajinyima haki ya
kuomba ridhaa ya kugombea kupitia Chama cha Mapinduzi,"alisema Nape.
Katiba ya chama.Kinyume cha hapo watakuwa wanajinyima haki ya
kuomba ridhaa ya kugombea kupitia Chama cha Mapinduzi,"alisema Nape.