Emmanuel okwi akimsii niyonzima atoke uwanjani
Niyonzima akimwambia meneja wa timu hiyo kuwa asikii
Niyonzima akimwambia meneja wa timu hiyo kuwa asikii
Na Humphrey Shao, Dar es Salaam
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Uganda anayekipiga katika klabu
ya Simba, Emmanuel Okwi, amemsababishia kiungo wa Yanga,Haruna Niyonzima kupata
tatizo la kutosikia Filimbi ya mwamuzi
kutokana na kelele za Mashabiki.
Niyonzima ambaye alitolewa nje kwa kadi nyekundu kutokana na
kupiga mpira wavuni kisha kumlalamikia
mwamuzikuwa alikuwa sikii nini kinaendelea akiwa mchezo kutokana Mashabiki wa
Simba walikuwa wanashangilia sana.
“kiukweli nilikuwa sisikii hiyo filimbi ya mwamuzi kwani awa
mashabiki wa Simba wana kelele sana kiasi cha kunichanganya sasa sioni sababu
ya mwamuzi kunipa kadi nyekundu wakati nimemweleza sikusikia kutokana na kelele
za mashabiki” alisema Niyonzima.
Niyonzima altoka uwanja huku akiongea maneno ya kejeli huku
akitukana matusi kwa waamuzi juu ya kile alichotendewa na mwamuzi wa kati wa
mchezo huo.
mwisho