Mwanamuziki wa Injili kutoka Tanzania Rose Muhando ameleta utata
mtandaoni baada ya kutoa sifa za kuonyesha kumkubali Mwanamuziki wa
Bongo Fleva H-Baba kwa kazi yake mpya Show Time,Rose Mhando alitoa sifa
hizo baada
Msanii wa Bongo Fleva H Baba akiwa na Mwibaji wa nyimbo za injili Tanzania Rose Mhando.
ya kushuhudia show aliofanya H Baba na wimbo wake mpya wa Show Time.
Rose Mhando alinukuliwa akisema kuwa show aliyoiona kwa H Baba na huo
wimbo wake mpya ni matata sana na kama akiendelea kutoa nyimbo kama hiyo
hakika wasanii wenzake
wanatashidana sana lakini hawataweza kumfikia,lakini pia aliongeza kuwa H
Baba ni msanii ambae anakuwa toka alipoanza kutoka na Mpenzi Bubu
amekuwa anazidi kupanda
hata show zake ni matata sana ukilinganisha na show zingine za wasanii wa bongo fleva.
Baada ya watu kuonyesha hawajapendezwa na kitendo alichokifanya
mwanamuziki huyo wa Injili kukubali nyimbo za kidunia H baba alisema
kuwa Rose Mhando ni mwanamuziki
mwenzake hivyo haoni kama kuna ubaya yeye kumsifia kwani alichosifia
amesifia sanaa yake na si kitu kingine hivyo hakuna tatizo lolote.
"Namkubali sana Mwanamuziki wa injili Rose Mhando kwakuongea ukweli
kutoka moyoni.Naomba niulize Kwakuwa amesifiwa H.baba ndio kakosea
mlitamani asifiwe nani sasa apo
ukweli utabakia Kuwa ukweli siku zote toka Mpenzi bubu,mpaka Leo nipo
nijambo lakumshukuru muumba.sasa Rose ni mwanamuziki mwenzangu kunisifia
nisawa tuu mbona disco
wanapiga nyimbo za Makoma kwani wale wanaimba mziki wakidunia?" Alihoji H-Baba.
"Hebu punguzeni kelele Rose Mhando amenisifia baada yakuona Show yangu
wimbo nilioimba ukamvutia ni Show Time na upande wa Show pia jukwanii
hilo linafahamika ila
linachengeshwa kila siku ila Mungu ananisimamia nipo mpaka leo,Mbona
Alli Kiba amesifia show zangu hamjaongea kitu,hii imeingia kwenye
historia ya nchi tayari.Ahsante
dada angu Rose Mhando nakukubali sanaa." Aliongeza H-Baba.
Kutokana na hili mwanamuziki wa Rap kutoka mwanza Fid Q kwa upande wake
aliibuka na kusema kuwa hata yeye anaungana na mwanadada Rose Mhando
kwani anamkubali sana H
Baba kwa show zake na nyimbo zake pia hali ambayo ilimfanya Fid aanze
kutoa mwongozo kwa mashabiki wake ambao nao walionekana kupokea tofauti
ujumbe wa Rose Mhando juu
ya kumkubali H baba na kuanza kumuhukumu kwa mambo mbalimbali na ufuatao
ulikuwa ufafanuzi wa Fid Q kwa watu ambao wameweza kumjudge Rose Mhando
juu ya kauli yake ya
kumkubali H baba.
"Nashukuru tumekubaliana katika suala la mwenye mamlaka ya hukumu..Joa
lyimo sasa tubaki katika tafsiri ya UPENDO.. Sasa kama dada hatompenda
ndugu yake anayemuona..
Atawezaje kumpenda Mungu asiyemuona? Ni ukweli tumeonywa kuhusu anasa za
kidunia lakini pia tusisahau kama tunauhitaji msaada wa mwenye dhambi
ili kumfukuza
shetani.Eliud Nyaulingo Lakini Kaisali ni kiumbe wa Mungu pia.. Huenda
UPENDO huu alioonyeshwa ukamvutia kiasi cha yeye kurudi kundini..
Haudhani?"