Naibu waziri
wa Viwanda na Biashara , Janeth Mbene, akizungumza na Meneja wa Mamlaka ya
mapato mkoa wa Mbeya, Joseph Ruge, katika ofis za TRA Kasumulu. Picha na
Humphrey Shao
Na Humphrey
Shao, Kyela
MPAKA wa
Kasumulu ni moja ya mipaka ambayo
inaingiza fedha nyingi katika serikali kupitia kodi ya mapato na tozo
mbalimbali, mpaka huu una urefu wa kilometa 32 kutoka wilaya ya Ileje upande
magharibi hadi ziwa Nyasa upande wa mashariki katika wilaya ya Kyela.
Mpaka huu
ambao una vivuko visivyo rasmi vipatavyo 32 ambavyo hutumika kuvusha bidhaa za magendo ambazo uchangia kwa
kiasi kikubwa kupotea kwa mapato na bidhaa ambazo azina viwango kwa matumizi
hapa nchini
Hivi
karibuni Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Janeth Mbene, akiwa na maofisa
waandamizi wa shirika la Viwango nchini(TBS),walitembelea mpaka huo hili
kujionea namna shughuli zinavyofanyika katika mpka huo.
Akiwa katika
mpaka huo Waziri mbene aliweza kujionea na namna tasisi mbalimbali zinavyofanya
kazi na kupata ripoti ya tasisi mama katika eneo hilo mamlaka ya mapato
nchini(TRA).
Waziri Mbene
alibaini kuwa licha ya kuwepo tasisi kadhaa za serikali katika eneo hilo lakini
bado kuna upungufu wa kutokuwepo kwa shirika la viwango nchini(TBS) Katika eneo
hilo hali inayo hatarisha maisha ya walaji wa bidhaa zianazopita katika mpaka
huo licha ya kulipiwa ushuru.
Waziri mbene
amelitaka shirika la Viwango Tanzania (TBS) Kuakikisha kuwa wanaweka kituo cha
ukaguzi katika mpaka wa Kasumulu kwa haraka katika eneo hilo kutokana na
mahitaji ya mpaka huo ambao upitisha bidha akutoka nchi za Malawi na Afrika
Kusini.
Mbene
anasema kuwa kumekuwa na tatizo la kusambaa kwa bidhaa katika masoko ya nyanda
za juu kusini ambayo yanapitishwa katika mpaka wa Kasumulu hali inayochangia
kwa bidhaa za ndani kukosa masoko .
“Serikali
yote iko hapa hivyo ni aibu kuona kuwa atuna kituo cha tbs katika mpaka huu
kwani hii ni moja ya lango kuu la uingizaji bidhaa kwa ajili ya mikoa ya nyanda
za juu kusini kutokea nchi jirani ya Malawi na Afrika kusini kama nilivyoelezwa
kwenye ripoti ya TRA” alisema Waziri Mbene.
Akieleza
mbele ya naibu waziri Afisa habari wa
TBS, Roida Andusamile, alisema kuwa shirika hilo lipo katika mchakato wa kuweka
kituo katika kituo hicho hili kupunguza tatizo la uingizwaji wa bidhaa ambazo
azikidhi viwango.
Roida
anasema kuwa wao kama maofisa wa TBS wameona namna mpka huo ulivyokuwa na
umuhimu wa kuwekewa kituo cha ukaguzi kama ilivyo katika bandari na vituo
vingine kwani biashara ya bidhaa na vyakula ni kubwa kuliko kawaida.
Kwa upande
wake Kaimu afisa mfawidhi forodha Kasumulu Delya Yohana anasema katika kipindi
chote wamekuwa katika mapambano makali juu ya uingizwaji wa pombe za viroba
kutoka nchini Malawi.
Anasema kuna
kila sababu ya TBS kuwepo kwani bidhaa za vilelevi zimekuwa zikiingia na
kulipiwa ushuru licha ya baadhi kupigwa marufuku kutokana na uwepo tasisi ya
chakula na lishe ya TFDA kubaini kuwa vina kemikali mbaya.
Alitaja kuwa
idadi ya magari yanayoingia katika kituo hicho kuanzia mwezi Desemba ni magari
yaliyoingia ni 1389 na yaliyotoka ni 592 na thamni ya mizigo iliyokwenda nje
kama export ilikuwa sh11,833,414,899.
Alitaja kuwa
kudorola kwa uchumi wa Malawi kumechangia kwa kiasi kikubwa kushuka kwa
baishara katika mpaka huo ambao unategemewa kama lango kwa nchi jirani.
Alitaja kuwa
mizigo inayotoka nje ya nchi na bidhaa zinazouzwa nchini Malawi ni Saruji
kutoka mbeya , Sabuni,bidhaa za majumbani,Mafuta ya kupaka, Mafuta ya kupikia
na Juice za Azam.
Mizigo
inayoingia nchini kwa wingi ni vipuri vya Viwandani hasa vile vya kiwanda cha
Sukari cha Kilombero, bidhaa zingine ni mbao kutoka nchini Malawi, Mashudu ya
kulishia wanyama na Vipodozi.
Anasema kuna
mpango wa kujenga kituo kimoja cha Forodha kijulikanacho kama OSBP(One stop
Border Post) Katika mpaka wa Kasumulu Faida ya mradi huu ni pamoja na kupunguza
muda wa kuingiza na kutoa mizigo na kudhibiti magendo ulinzi na usalama
mpakani.
mwisho