THE UNITED
REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512,
2116898
E-mail: ikulucommpress@googlemail.com
Website : www.ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425 |
|
PRESIDENT’S OFFICE,
STATE
HOUSE,
1 BARACK OBAMA ROAD,
11400
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA KWA VYOMBO
VYA HABARI
Rais
Kikwete aiomba India kugharamia ujenzi wa reli ya Dar es Salaam
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ameiomba
Serikali ya India kukubali kugharamia ujenzi wa reli katika Jiji laDar es Salaam ili kupunguza
misongamano mikubwa ya magari na kuongeza usafisi wa usafiri katika Jiji hilo.
Ombi
hilo la Serikali ya Tanzania limetolewa na Rais Kikwete asubuhi ya leo, Ijumaa,
Juni 19, 2015, wakati alipokutana kwa mazungumzo rasmi na Waziri Mkuu wa India,
Mheshimiwa Narendra Modi, ikiwa ni sehemu ya shughuli za Rais Kikwete kwenye
ziara yake rasmi ya Kiserikali ya siku nne katika India kwa mwaliko wa Rais wa
nchi hiyo, Mheshimiwa Pranad Mukherjee.
Katika
mazungumzo hayo, Rais Kikwete amemweleza Waziri Mkuu Modi kuhusu jinsi wingi wa
magari ulivyoongeza misongamano mikubwa ya magari na hivyo kupunguza sana
ufanisi wa usafiri kwa mamilioni ya wakazi wa Jiji hilo. Inakadiriwa kuwa Mji
wa Dar Es Salaam una wakazi zaidi ya milioni nne kwa sasa.
Katika
maelezo yake, Rais Kikwete ameiomba Serikali ya Modi kufikiria uwezekano wa
kugharamia ujenzi wa reli ya juu ya ardhi (siyo ya chini ya ardhi) kama njia ya
uhakika zaidi ya kupunguza misongano.
Rais
Kikwete amemwambia Waziri Mkuu kuwa tayari amezungumza na Kampuni ya Infrastructure
Leasing and Financial Services (IFLS) ya
India ambayo imeonyesha hamu ya kushiriki katika ujenzi wa reli hiyo kwa nia ya
kuongeza ufanisi wa usafiri kwa wakazi wa Dar es Salaam.
Jana,
Alhamisi, Juni 18, 2015, miongoni mwa watu wengine, Rais Kikwete alifanya
mazungumzo na Mwenyekiti wa ILFS, Bwana Ravi Parthasarathy kuhusu ujenzi wa
reli hiyo na Mwenyekiti huyo akaonyesha hamu kubwa ya kufanya hivyo ili mradi
Serikali ya India ishauriwe na kukubali kugharamia mradi huo.
wakati huo huo Serikali
ya India imesema kuwa iko tayari kuongeza nafasi na fursa za raslimali fedha na
nafasi kwa Tanzania katika maeneo mbalimbali yakiwemo elimu, afya,
kilimo, ulinzi na mapambano dhidi ya ugaidi.
Aidha,
Serikali ya India imesema kuwa itaanzisha utaratibu ambako Watanzania wanaoomba
visa za kuingia India kwa ajili ya matibabu sasa wanaweza kuomba na kupata visa
hizo kwa njia ya mtandao (e-visa).
Hatua
hizo za Serikali ya India kwa Tanzania zimetangazwa leo, Ijumaa, Juni 19, 2015,
wakati Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Mheshimiwa Narendra Modi alipokutana kwa
mazungumzo rasmi ya Kiserikali na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ambaye yuko katika ziara rasmi ya siku nne
nchini India kwa mwaliko wa Rais Pranab Mukherjee.
Katika
mazungumzo hayo yaliyofanyika Hyderabad, Waziri Mkuu ambaye ndiye kiongozi wa
Serikali katika India alisema kuwa Serikali yake iko tayari kupokea na
kutafakari maombi mapya ya Tanzania katika maeneo ya ushirikiano wa kijeshi
kama Tanzania inahitaji kuimarisha zaidi majeshi yake na shughuli za ulinzi
katika dunia ya sasa iliyobadilika sana.
Amesema
kuwa India iko tayari kupokea na kutafakari maombi ya ushirikiano wa pamoja
katika maeneo ya usalama wa bahari hasa katika kukabiliana na tishio la ugaidi
katika Bahari ya Hindi.
Waziri
Mkuu pia amesema kuwa India iko tayari kuongeza nafasi za masomo kwa Tanzania
na wanafunzi wake. Mpaka sasa, kiasi cha wanafunzi 2,000 wanasoma katika vyuo
vikuu na taasisi nyingine za elimu ya juu katika India.
“Tuko
tayari kuongeza nafasi za masomo na elimu na katika maeneo mengine ya ujenzi wa
uwezo wa Watanzania,” amesema Waziri huyo.
Kuhusu
upatikanaji wa visa kwa Watanzania ambao wanataka kuingia katika India kwa
ajili ya kupata matibabu, Mheshimiwa
Modi amesema kuwa India imekubali kuwa Watanzania wanaotaka huduma za tiba,
wataweza kuomba visa kwa kutumia njia ya mitandao na hivyo kupata visa haraka
zaidi kuliko sasa.
Mara
baada ya mazungumzo hayo, viongozi hao wawili wamehudhuria mkutano na waandishi
wa habari ambako wameshuhudia utiaji saini mikataba minane ya ushirikiano kati
ya Tanzania na India.
Mapema
leo asubuhi, Rais Kikwete alipokelewa rasmi na Rais Mukherjee katika sherehe
zilizofanyika kwenye Ikulu ya India ya Rashtrapati Bhavan, sherehe ambayo pia
imehudhuriwa na Waziri Mkuu Modi.
Rais
Kikwete amepigiwa mizinga 12 na kukagua gwaride kwa heshima yake katika sherehe
hiyo iliyochukua kiasi cha dakika 10. Baada ya sherehe hiyo, Rais Kikwete
ametembelea Jumba la Kumbukumbu Mahatma Gandhi la Rajghat lililoko mjini New
Delhi.
Rais
Kikwete pia amekutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa India,
Mheshimiwa Sashma Swaraj katika mazungumzo yaliyofanyika kwenye Hoteli ya Taj
Palace ambako Rais Kikwete na ujumbe wake amefikia.
Rais
Kikwete pia amekutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa India,
Mheshimiwa Mohammad Hamid Ansari na
Waziri wa Afya na Ustawi wa Familia, Mheshimiwa J.P Nadda.
Baadaye
jioni, Rais Kikwete alitarajiwa
kuhudhuria dhifa ya kitaifa iliyokuwa inaandaliwa kwa heshima yake na Rais
Mukherjee.
Imetolewa na;
Kurugenzi ya
Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
19 Juni, 2015