MKURUGENZI Mtendaji
wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku, amesema katika muda huu wa
kuelekea uchaguzi mkuu ni vema watanzania watazamane nani ni nani na alifanya
nini katika nchi hii.
Aliyasema hayo jana katika mkutano wa amani ulioandaliwa na
taasisi hiyo na kufanyika katika ukumbi wa Blue Pearl jijini Dar es Salaam
ambapo ulihudhuriwa na wananchi mbalimbali wakiongozwa na watoa mada ambao ni
pamoja na Butiku, mjumbe wa bodi ya wadhamini wa taasisi hiyo, Getrude Mongela
na Humphrey Polepole ambaye ni mjumbe.
Akitolea mfano wa kashfa iliyotokea kwenye serikali
inayomaliza muda wake Butiku alisema watu wamekuwa wakijadili kuhusu
uwajibikaji na kusema kuwa mtu fulani (hakumtaja jina) aliwajibika ili kumwokoa
rais wake na serikali yake lakini bado watu hawafahamu ukweli.
Hata hivyo alisema “ubishi” huo ulitakiwa kuanza mapema na
si wakati huu wa uchaguzi ambapo kila mtu anafanya jambo ili aweze kupata
madaraka.
“Ubishi huu ulistahili kujitokeza mapema na si sasa hivi”
alisema Butiku na kuongeza kuwa uwajibikaji umekuwa si wa viongozi bali ni wa
taasisi suala ambalo alipingana nalo kwa kusema viongozi ndio wanaotakiwa
kuwajibika.
“Sasa hivi watu wamekuwa wakizungumzia taasisi utasikia CCM
(Chama cha Mapinduzi), Chadema (Chama cha Demokrasia na Maendeleo), NCCR
Mageuzi, CUF na vingine lakini viongozi ndio wakuwajibika na hawana namana ya
kukwepa ukweli huu.
Alisema viongozi wasikwepe wajibu wao kwasababu wao ndio
hukabidhiwa dhamana ya kushughulikia umaskini, rushwa na ufisadi, viongozi wanaochaguliwa
katika chaguzi zote zilizopita na huu unaokuja ndio ambao awali waliwahi kukabidhiwa
dhamana ya uongozi na baadhi yao ndio leo wanaoomba nafasi za uongozi ili
wasaidiane na wananchi kusimamia mambo yote ya wananchi.
“Kukubali kuwajibika ndio badiliko la msingi linalotakiwa
sasa, kujaribu kukwepa uwajibikaji ama wa kiongozi binafsi au wa uongozi wa
pamoja hasa katika ngazi ya taifa ndiyo dalilili ya uhakika ya kukataa
mabadiliko. Falsafa ya uongozi inasema kuongoza ni kuonyesha njia na ili
kuongoza ni lazima kuwa mbele na kuonyesha mfano na kiongozi mzuri ni yule
anayeonyesha njia. Tujifunze kujua wananchi wanataka nini ili iwe rahisi
kuwaongoza,” alisem Butiku.
Alisema mapungufu yaliyopita na yaliyopo katikka
kuwahudumia watanzania yanatokana na mapungufu ya viongozi mmoja mmoja na
katika umoja wao ambapo aliongeza kuwa uwajibikaji katika mapunguufu hayo ni wa
viongozi na si wa chama au serikali.
Aidha aliwataka wananchi kutowaamini watu wanaoomba ridhaa
ya kuongoza na wanafanya kila jitihada kukwepa wajibu wao binafsi au wa kundi
lao la uongozi wa pamoja na kusema kuwa viongozi wa ain ahiyo hawafai.
Alisema viongozi wengi wamejenga tabia na hulka ya
kuwahutubia wananchi badala ya kuwapatia utaalam, zana za kisasa za kilimo,
kuwapa ardhi na kuwapimia, kuweka mipango ya kilimo cha umwagiliaji, ufagaji n
auvuvi wa kisasa, kujenga viwanda vikubwa na vidogo na hasa vile vya kusindikia
mazao ya wakulima ili kuongeza thamani ya bidhaa za kilimo.
“Hili ni tatizo la uwajibikaji na kukubali ukweli wote
kuhusu uwajibikaji. Viongozi waliopita na waliopo kwa miaka yote 54 ya uhuru wa
nchi yetu ukiondoa vijana wa miaka 18 iliyopita walikuwepo,” alisema Butiku na
kuhoji nani amlaumu nani ikiwa viongozi hao waliokuwepo na waliotoka ndani ya
chama hicho wapo?
Aidha alisema hakuna wakumnyooshea kidole mwenzake
kwasababu wote walishiriki katika uamuzi na utekelezaji na kwamba hakuna
aliyewahi kuwajibika.
“Rushwa na ufisadi umekuwepo kwa miaka mingi kadhalika
matatizo ya ardhi, elimu, afya, maji na ajira. Naniu aliwahi kujiuzulu wadhifa
wake kwa kutoridhika na utekelezaji ndani ya chama au serikali?” alihoji
Butiku.
MONGELA
Kwa upande wake Mongela alianza kutoa mada yake kwa kusema
anawashangaa watu wanaosema hawawezi kuongozwa na wazee kama yeye lakini bado
kuna wazee wanagombea nafasi ya urais.
Aidha alisisistiza kuwa mabadiliko lazima yaletwe na vijana
na si wazee waliochoka midhili yake.
“Kama mnatafuta watu wakuongoza mabadiliko tafuteni vijana,
wazee kama sisi tumeshachoka na muda wetu umekwisha,” alisema Mongela.
Akizungumzia suala la amani alisema Tanzania ilikuwa
maskini na sasa ni maskini lakini amani bado ipo na kuhoji kama ni sahihi kuwa
maskini ambao hawana amani.
“Tulikotoka tulikuwa masikini na tulikuwa na amani,
tukaendelea na umasikini haujaisha lakini tupo na amani. Je mnataka hata amani
tuipoteze?” alihoji Mongella na kutolea mfano taifa la Misri ambapo alisem
awaliandamana na kumtoa kiongozi wao kwa fujo na sasa wanapinduana kwasababu
walifanya mabadiliko bila kufikiria.
Kuhusu uchaguzi alisema ndiyo sehemu sahihi ya kufanya
mabadiliko lakini akataatharisha kutofanya mabadiliko ya hasira na yasiyo na
amani.
“Tunaenda katika uchaguzi na uchaguzi kuna uchungu na
wasiwasi wa kutochaguliwa na watu wenye wasiwasi hawana amani na mtu wa namna hiyo
hawezi kuwa na heshima. Lazima tuwe na utii wa sheria na kila mtu akitekeleza
wajibu wake tutakuwa na uchaguzi wa amani,” alisema Mongella.
TASLIMA
Akichangia mjadala katika mdahalo huo Mbunge wa Bunge la
Afrika Mashariki na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF, Twaha Taslima, alitoa
ujumbe wan chi za afrika mashariki na kusema wanaiombea amani Tanzania
kwasababu ndiyo nchi iliyopakana nan chi zote za Afrika.
Aidha aliitaka Tume tya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kutenda
haki kwenye uchaguzi ujao kwani kinyume na kufanya hivyo amni iliyopo inaweza
kutoweka japo hakun aanyetaka iwe hivyo.
Aidha aliishauri tume kuairisha uchaguzi pale ambapo itaona
mambo hayaendi vizuri ili kuinusuru amani iliyopo.
“Nimekuja hapa kuleta ujumbe wa nchi za Afrika Mashariki,
wanatuombea amani kwasababu tumezungukwa nan chi zote za Afrika Mashariki n
atumekuwa na mchango mkubwa katika kurudisha amni kwenye nchi zao, tunaomba NEC
isaidie kuhakikisha amani hii inakuwepo kwa kutenda haki na pale inapoona mambo
hayaendi vizuri ni bora wakahairisha uchaguzi sisi tupo tayari,” alisema
Taslima.
Kwa upande wake Humphrey Pole pole ambaye ni miongoni mwa
washiriki wa taasisi hiyo, alisema kushindwa kuwajibika na kuwambana na ukweli
mwisho wake uwendea uongo na kudai
kwamba kufanya hivyo heshima haitakuwapo.
“Ustahimilivu wetu haupo tena, siku hizi ukisema kitu
ambacho mwingine hataki kusikiliza na matokeo yake utatolewa lugha chafu tabia
ambayo hipo kwenye mitandao ya kijamii,”alisema Pole pole.
Alimnukuu Mwalimu Nyerere kwa kusema kwamba aliubiri siasa
safi na uongozi bora na kutolea mfano wa baadhi ya wanachama wa vyama
mbalimbali nchini kwa tabia ya kuzomea wengine barabarani na kudai kwamba kwa
kufanya hivyo ni kuwanyima uhuru wa maamuzi huku viongozi wakikaa kimya bila ya
kukemea jambo hilo.
Alisema hafurahishwi na anayoyaona leo katika maisha yake tabia
ya viongozi kumungunya maneno huku wakiendelea kuhubili uongo kwa kudai kwamba
haelewi utokea kwa lengo gani.
“Uongo ni adui yetu mkubwa, tulipokuwa tuki yasema hayo
hapo awali wenzetu walitutukana tukiwa na mzee
wetu Butiku kuwaeleza kwamba tunamatatizo na kujaribu kuwa uma sikio juu
ya hilo.
Alisema kwamba aliwahi kusema kwamba endapo CCM
wangemchagua fisadi angezunguka nchi
nzima kupinga jambo hilo na kujaribu kutolea
muktadha wa Mwalimu Nyerere wa mwaka 1995 kwa kudai kwamba kwa wakati
huo wananchi walichoka na rushwa na kuongezea kuwa uongozi si utajiri, ukabila,
udini na kuwataka wapiga kura kuwatathimini wagombea wao.
“Tuwanze kwa kusema kijiko ni kijiko na bereshi si kijiko
kikubwa, nikiona mtu ndani ya CCM
ameyazuia maoni ya wananchi niko lazi kupambana nae.
“Televisheni tatu wamesema Polepole nisiende kwenye mijadala yao, leo hii kuna magazeti
hazitoi makala zangu,”alisema na kuongezea kwamba kushindwa kwa vyama vya
upinzani kutekeleza ajenda ya ufisadi ambayo ndio ajenda ya taifa na CCM
kujitutumua kwa kufungua mahakama ya ufisadi ndio mabadiliko ambayo kwa upande
wa vitabu vya dini tukio hilo linahashiria kuwa ni siku ya mwisho umewadia.
Pia alikemea kauli za kichochezi kwa vyama vyote ambapo
alitolea mfano kauli ya ‘Bao la Mkono’ iliyotolewa na Katibu Mwenezi wa CCM
Nape Nnauye, kwenye mkutano wa kampeni Mtwara na ile ya UKAWA, Tanganyika
Packers kuwa si nzuri.
“Baada ya kauli ile nilimkanya Nape lakini sikumuona
kiongozi aliyejitokeza na kukemea ile kauli ya ikiwa kama uchaguzi utakuwa
uhuru na haki CCM ijiandae kukabidhi Ikulu na kama wakikataa watatumia nguvu ya
umma kwenda Ikulu
“Kwenda kudai Ikulu kwa nguvu ya umma kwenye sheria ni kitu
gani kitatokea?,”alisema Polepole.
Akihitimisha mdahalo huo Butiku aliwatahadharisha vijana
kuwaepuka wazee wanaowachonganisha badala ya kuwaeleza ukweli na kudai kuwa
wazee wanaohama miji saa za mwisho wanamatatizo.
“Ukiona baba au babu anahangaika saa za mwisho na kuhama
mji ujue huyo ana matatizo, wazee si watu wakuchonganisha bali ni watu
wakupatanisha sasa wazee wamekuwa wachonganishi badala ya kuwaeleza ukweli,”
alisema Butiku.
Alisema vijana wanaweza kuvaa mashati ya vyama lakini
watafute ukweli na baada ya kujua ukweli wakafanye uamuzi kwa kuangalia dhamira
zao.
“Vaeni mashati ya vyama lakini tafuteni ukweli wa mambo na
mkishaujua ukweli mkafanye uamuzi kwa kuangalia dhamira zenu…mtu ukifanya
uamuzi bila kuangalia dhamira yako kesho yake usimlaumu mtu,” alisema Butiku.