Mourinho
atupiwa virago Chelsea
LONDON England
CHELSEA hatimaye imefikia uamuzi mgumu kabisa wa
kumtimua kocha wao kipenzi, Jose Mourinho ikiwa ni miezi saba tu tangu kocha
huyo aimbiwe wimbo wa kishujaa baada ya kuiwezesha timu hiyo kutwaa ubingwa wa
England.
Uamuzi wa Bodi ya Chelsea umetangazwa jana jioni na
umeelezwa kuchangiwa na matokeo mabaya ya timu hiyo katika Ligi Kuu ya England
(EPL) msimu huu, ambapo timu hiyo inashika nafasi ya 16 ikiwa na pointi 15
kutokana na michezo 16 iliyocheza.
Kufungwa na vinara wa ligi hiyo Leicester City mabao
2-1 na kuwafanya wawe nyuma kwa pointi 20 nyuma ya timu hiyo, kulimfanya mmiliki
wa Chelsea, Roman Abromovic kuitisha
kikao cha bodi ambacho kwa pamoja kilifikia uamuzi mgumu licha ya malalamiko ya
kocha huyo aliyoyatoa kwamba anahujumiwa na wachezaji wake.