PENGO AJITOKEZA KUZUNGUMZIA AFYA YAKE



ASKOFU Mkuu wa Kanisa Katoliki nchini, Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo amejitokeza kwa mara ya kwanza na kuzungumza juu hali yake.
kardinali Pengo alilazwa JCKI Desemba 31, mwaka jana ambapo aliushukuru uongozi wa hosptali hiyo kwa matibabu aliyoyapata na kwamba sasa anaendelea vizuri na anaweza kutoka wakati wowote kuanzia sasa.
“Siku hizi nimepoteza maneno siwezi kuzungumza sana… lakini napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa wahudumu walionisaidia tangu nilipofikishwa hapa.
“Kwangu imekuwa nafasi nzuri kuifahamu Hospitali ya Muhimbili, nawaomba waandishi wa habari muwe mnaandika pia na mazuri yaliyoko hapa maana mimi ni mmoja wa watu niliokuwa naamini kwamba hakuna huduma nzuri, semeni ukweli,” alisema.
Kardinali Pengo alitoa zawadi ya kadi kwa baadhi ya wakuu wa vitengo vya hospitali hiyo ikiwamo Idara ya Dharura (Emergence), JCKI na Idara ya matumbo kama sehemu ya shukurani yake.
Naye Kaimu Mkurugenzi wa JCKI, Profesa Mohamed Janabi alisema hali ya Kardinali Pengo inaridhisha kwa sasa na kwamba atapatiwa ruhusa mwishoni mwa wiki hii.
“Hapa tunashughulikia maradhi ya moyo, Askofu alikuwa akisumbuliwa na tatizo la moyo na wamelishughulikia hivyo ataruhusiwa mwishoni mwa wiki hii.
MWISHO

Post a Comment

Previous Post Next Post