MSANII wa Bongo Fleva, Benard Paul ‘Ben Paul’, amesema hapendi na hatauchora ‘tattoo’ mwili wake
kama baadhi ya wasanii na watu maarufu wafanyavyo kwa kuwa anauheshimu sana.
Ben Paul alisema imekuwa ni kawaida kwa idadi kubwa ya
wasanii kujichora ‘tattoo’ na kuwa na mwonekano wa tofauti na watu wengine,
lakini kwake jambo hilo halina nafasi.
“Japo ni msanii lakini sipendi kuwa na mwonekano wa tofauti
kama kufuga rasta, kuvaa hereni au kujichora mwilini kwa sababu nauheshimu mwili
wangu, ndiyo maana nipo kawaida kila wakati,” alifafanua.