MWIMBAJI wa nyimbo za injili nchini,
George Kayala amezidi kujitanua kwa mashabiki wake baada ya kuanzisha ‘group’
maalumu la whatsapp linaowahusisha wale wote walioguswa na albamu yake mpya ya Maajabu
ya Damu ya Yesu.
Akizungumza na jijiletu jana, Kayala alisema kwamba watu wengi
wameguswa na nyimbo zilizomo ndani ya albamu hiyo na ili kuhakikisha anajenga
mahusiano mazuri nao ndipo akaanzisha group hilo alililolipa jina la Maombi ni
Silaha.
“Nimelazimika kutoa nyimbo zangu bure
kwa mashabiki wangu ndani na nje ya nchi kwa njia ya whatsapp na wengi wameguswa
na vibao hivyo, na ili nisiwapoteze ndipo nikaamua kuunda group hili ambalo pia
linatumika kwa kuombea mahitaji mbalimbali ya wadau hao,” alisema Kayala.
Kayala alisema kwamba mashabiki wake
wengi amewapata kwa njia ya facebook ambako amekuwa akiwajulisha nini
kinachoendelea juu ya huduma yake hii ya uimbaji.