Malkia wa muziki wa Taarab nchini
Khadija Kopa amesema sababu ambayo inasababisha
soko la muziki wa taarab kushuka na kutochezwa kwa wingi kwenye radio na
ruringa ni moja ya sababu kubwa inayoifanya
kuanguka kwa muziki huo, pia wasanii wa taarab kutokwenda na wakati
kuwa mbunifu zaidi kwenye utunzi wa
nyimbo.
Akizungumza na MTANZANIA amesema
kuwa kwa sasa muziki wa Bongo
fleva ndio umeshika nafasi ya kuwa juu kuliko muziki wa taarab na sababu kubwa
ni vyombo vya habari na wasanii wa taarab kutokujituma zaidi kwenye utunzi wa
mashairi na kujua mashabiki wanataka nini kwa wataki huu.
“Muziki wa taarab unashuka kwa
sababu ya vyombo vya habari kuwapapromo zaidi muziki wa kizazi kipya ukwel
muziki wa taarab bila vyombo vya habari
hatuwezi kufika popote, hapa tulipofikia sisi wengine mpaka tunazeeka ni nguvu
za vyombo za habari bila waotusingefika hapa tulipo sasa,” alisema Khadija
Kopa.
Aliongezea na kusema kuwa anaomba
serikali kuwasaidia kuwashika watu wanaonakili kazi zao na kuzipiga kwenye
masherehe mbalimbali huku wao kukosa show.