DIAMOND ALISIMAMISHA BUNGE

MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Nassib Abdul ‘Diamond’, jana amelisimamisha Bunge baada ya kutambulishwa na Spika wa Bunge, Job Ndugai, kuwa ni moja ya wageni waliohudhuria bungeni.
Diamond ambaye alikuwa ameambata na wageni wake kutoka kundi la Mafiki Zolo la nchini Afrika Kusini, baada ya kutambulishwa wabunge walishindwa kuzuia hisia zao na kujikuta wakimshangilia kwa nguvu mwanamuzi huyo.
Wasanii hao ambao waliingia bungeni kwa mwaliko wa Waziri wa Habari, Utamaduni, Michezo na Sanaa, Nape Nnauye.
“Waheshimiwa wabunge kuna tangazo la wageni hapa, leo tumetembelewa na wageni mashuhuri humu ndani, sio wengine ni wanamuziki wa kundi la Mafikizolo.
“Lakini hawa wameongozana na mwenyeji wao, kijana wetu anayeitangaza nchi huko duniani, wapo na Nasib Abdul au Diamond,” alisema Spika Ndugai
Spika alisema kwamba mbali na wasanii hao pia Diamond amekuja na Meneja wake Babu Tale.
Baada ya tangazo hilo, ukumbi wa Bunge ulilipuka kwa furaha baada ya wabunge, wageni na waandishi wa habari waliokuwepo ukumbini hapo kugeuka upande aliokuwepo mwanamuziki huyo ili wamuone.
Nderemo hizo zilidumu kwa dakika mbili hali iliyosababisha baadhi ya shughuli za Bunge sitishwa kwa muda huku waziri Nape akicheka na kushangilia.
“Ujio huu wa Diamond unatoa hamasa kwamba kuna kitu leo jioni kinafanyika, tunaomba waziri wa habari atutaarifu ili tujumuike pamoja,” alisema Spika Ndugai.
Baada ya maelezo hayo Bunge liliendelea na shughuli zake ambapo wabunge walikuwa wakichangia hoja kwenye Hotuba ya bajeti

Post a Comment

Previous Post Next Post