LUHWAVI AKAGUA UHAI WA CHAMA KWENYE MASHINA YA CCM WILAYANI KIHABA

 Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Lihwavi akizungumza na viongozi na wanachama wa CCM shina namba nne, la mjumbe Leticia Deodatus,  Kibaha mkoa wa Pwani, akiwa katika ziara ya kukagua na kuimarisha uhai wa Chama, jana. (Picha na Bashir Nkoromo).

--
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajabu Lhwavi akisalimiana na Mjumbe wa Shina namba tisa, tawi la KKKM, Kata ya Picha ya Ndege, Wilayani Kibaha mkoa wa Pwani, Bibie Lukemo, alipotembelea shina hilo, jana, kukagua uhai wa chama akiwa katika ziara ya kikazi wilayani humo. Katikati ni Mwenyekiti wa CCM Kata ya Picha ya Ndege. Mwalimu Mohammed Lukemo. (Picha na Bashir Nkoromo).
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajabu Luhwavi akipanda mti wa kumbukumbu katika eneo maalum ambalo viongozi wanaotembelea shina namba tisa, tawi la KKKM, Kata ya Picha ya Ndege kupanda mti kama huo, alipofika kwenye shina hilo, jana kukagua uhai wa Chama. (Picha na Bashir Nkoromo).
 Katibu wa CCM mkoa wa Pwani Joyce Masunga, akipanda mti wa kumbukumbu katika eneo maalum ambalo viongozi wanaotembelea shina namba tisa, tawi la KKKM, Kata ya Picha ya Ndege kupanda mti kama huo, alipofika na Naibu Katibu Mkuu wa CCM- Bara, Rajabu Luhwavi, kwenye shina hilo, jana kukagua uhai wa Chama. (Picha na Bashir Nkoromo).

 Mjumbe wa Shina namba tisa, tawi la CCM KKKM, kata ya Picha ya Ndege Kibaha mkoa wa Pwani, Bibie  Lukemo, akisoma taarifa ya shina hilo, Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rajab Luhwavi alipotembelea shina hilo kuimarisha na kukagua uhai wa chama jana. (Picha na Bashir Nkoromo).

 Wanachama wa CCM, Shina namba tisa, tawi la CCM KKKM kata ya Picha ya Ndege Kibaha mkoa wa Pwani, wakionyesha kadi zao za CCM, walipokuwa wanamshangilia Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Rajab Luhwavi alipotembelea shina hilo jana akiwa katika ziara ya kuimarisha na kukagua uhai wa Chama. (Picha na Bashir Nkoromo).
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi na Katibu wa CCM mkoa wa Pwani, Joyce Masunga, wakikagua daftari la wageni, walipokuwa nyumbani kwa amjumbe wa shina namba tatu, Tawi la Twende Pamoja, Kata ya Sofu, wilayani Kibaha mkoa wa Pwani,  Gasper Gama (kulia), Luhwavi alipotembelea shina hilo kukagua na kuimarisha uhai wa Chama, jana. (Picha na Bashir Nkoromo).

Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Lihwavi akizungumza na viongozi na wanachama wa CCM shina namba tatu, tawi la Twende Pamoja, Kata ya Sofu, wilaya ya Kibaha mkoa wa Pwani, akiwa katika ziara ya kukagua na kuimarisha uhai wa Chama, jana. (Picha na Bashir Nkoromo).

Post a Comment

Previous Post Next Post