Na Mwandishi
wetu
Mrembo
mwenye vipaji lukuki, Jokate Mwegelo kupitia kampeni yake yake ya kuchangia
jamii ijulikanayo kwa jina la “Be Kidotified” amejenga uwanja utakaotumika kwa
ajili ya michezo ya mpira wa kikapu na Pete (netiboli) kwa Shule ya Sekondari
ya Wasichana wa Jangwani.
Uwanja huo
ulizinduliwa jijini jana katika hafla fupi iliyofanyika kwenye shule hiyo na
kuhudhuriwa na wanafunzi, walimu na viongozi mbalimbali wa serikali. Ujenzi wa
uwanja huo umemgharimu Jokate kiasi cha Sh 50 milioni.
Akizungumza
katika uzinduzi huo, Jokate alisema kuwa ameamua kuonyesha mfano kupitia
‘Kidoti Brand’ kuchangia maendeleo ya michezo nchini hasa kwa katika shule
ambazo ni kiini cha maendeleo ya sekta hiyo hapa nchini. Mbali ya michezo, pia
Kidoti Brand inajihusisha zaidi na maendeleo ya elimu hapa nchini.
Alisema kuwa
serikali ya awamu ya tano ya Tanzania imeadhimia kuondoa changamoto nyingi
katika elimu na yeye kuamua kuanzia katika masuala ya michezo ambayo uchangia
ufaulu darasani na kuibua vipaji ambavyo vitamwezesha mshiriki kupata ajira.
Alisema kuwa
moja ya changamoto kubwa zinazorudisha nyuma maendeleo ya michezo nchini ni
ukosefu wa viwanja bora ambavyo ukwamisha wachezaji chipukizi kuonyesha vipaji
vyao ipasavyo.
Kwa mujibu
waJokate, alipokuwa anasoma, alikutana na changamoto hizo, lakini alipiga moyo
konde na kujihusisha na shughuli mbalimbali za nje ya darasa ikiwa pamoja na
michezo na kujifunza mengi.
“Mimi ni
mjasiriamali mchanga sana hapa nchini, nimehamasisha kwa kile kidogo
nilichonacho na kwa msaada wa wadhamini niliyotafuta kuhitimisha ujenzi wa
uwanja huu ambao utatumika si kwa wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Jangwani
pekee, bali hata kwa mechi za shule nyingine, ”
“Nawapongeza
wadhamini walioniunga mkono katika mpango huu kama Mo Dewji Foundation, na wadau
ambao walikuwa nyuma yangu katika kuhakikisha kampeni ya ‘Be Kidotified’ inaanza
kwa mafanikio makubwa na kuendelea kwa shule nyingine za hapa jijini,” alisema
Jokate.
Alisema kuwa
chapa ya Kidoti ni miongoni mwa chama zinazoongoza hapa nchini katika mitindo,
urembo na burudani kabla ya kuamua kupanua wigo kwa upande wa michezo tofauti
na mpira wa miguu.
Alifafanua
kuwa alianza kwa kuanzisha kampuni ya Kidoti
(Kidoti Company) na kuchangia katika soko la ajira nchini na baadaye kuanzisha “kidoti
brand’ akiwa na lengo la kuhamasisha vijana kujihusisha katika shughuli
mbalimbali za ujasiriamali ili kuweza kukabiliana na maisha ya kila siku.