SERIKALI YAKANUSHA JUU YA TUHUMA ZA WATANZANIA KUTESWA OMAN


 Wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imekanusha Taharifa zilizochapishwa na Gazeti la Tanzania Mpya yenye kichwa cha Habari kilichosema watanzania wateswa Oman na wengine na kunyofolewa figo zao na kupewa ndugu wa waajiri

akikanusha taharifa hiyo jijini Dar es Salaam leo Abdalah Kilima amesema kitendo hicho cha kuchapisha habari hiyo na kutumia picha ya Waziri Augistine Mahiga  hali iliyowanya watu wengi kuamini kuwa taharifa hiyo imetolewa na Wizara.
 "wizara inapenda kuwatangazia umma kwa ujumla kwamba mheshimiwa Dr Ausgustine Mahiga hausiki na taharifa hiyo na wala akuwahi kuzungumza na Mwandishi wa habari wa Makala husika na wala yaliyomo kwenye taharifa hiyo ni maoni binafsi ya mwandishi wa gazeti"alisema Balozi.





Post a Comment

Previous Post Next Post