Kocha msaidizi wa yanga Juma Mwambusi akiwa na kocha mkuu wa timu hiyo George Rwandamina wakipanga jambo katika mchezo wa dhidi ya Simba.
Na Humphrey
Shao, Globu Ya Jamii
Kocha msaidizi
wa klabu ya Yanga, Juma Mwambusi amekiri kuwa timu yake ilikuwa na tatizo
katika eneo la ukabaji na kupelekea kuchapwa bao 2-1.
Mwambusi
amesema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya
kumalizika kwa mchezo huo na kutaja ubovu wa timu yake.
“tulianza
mchezo huu vizuri lakini tatizo la ukabaji katika timu yetu ndio limetugharimu
na kuwapa wapinzani wetu ushindi wa wazi ambao kila mtu ameuona” amesema
Mwambusi.
Mwambusi
ametaja kuwa kulikuwa hakuna sababu ya timu yao kupoteza mchezo huo kwani
tayari walikuwa washatangulia kwa bao moja hivyo walikuwa na nafasi nzuri ya
kupata ushndi lakini uzembe wa wachezaji wachache umeigharimu timu.
Ametaja kuwa
tatizo lililowakuwa wapinzani wao la kupewa kadi Nyekundu lilikuwa zawadi tosha
ya kuondoka na ushindi lakini bado wachazaji walishindwa kukaba.