Matumizi ya
simu ya mkononi huku akiwa ameshikiliwa na jeshi la Polisi ni moja ya mambo
yalitojwa kumfanya mtuhumiwa wa kesi ya Dawa za kulevya Wema Sepetu kuendelea
kusota rumande.
Akizungumza na
waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo mkuu huyo wa mkoa amesema kuwa
moja ya makosa katika nchii hii ni mtu akiwa yupo chini ya ulinzi alafu
kuendelea kutumia simu ya mkononi.
Amesema kuwa
mrembo huyo ambaye alikuwa akituma Video na sauti mbalimbali kuhusu hali ya
maisha akiwa mahabusu ya kituo cha kati huku akimkejeli mkuu wa mkoa uenda
akaendelea kuwa katika wakati mgumu zaidi kutokana na kitendo hicho cha kutumia
simu akiwa mahabusu.
Makonda ametaja
kuwa amezungumza na wakuu wa magereza yote yaliyopo Dar es Salaam na wakuu wa
mikoa juu ya vitendo vya watu kuingia na simu katika vituo vya Polisi.
Pia amesema
kuwa matumizi ya simu hizo watu wakiwa gerezani yamekuwa yakitumika kuendeleza
biashara zao za dawa za kulevya kwa njia ya mawasiliano hata kama wakiwa ndani.