Msaidizi wa Rais wa shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, Juma Matandika akitoka mahakamani Mara baada ya kukutwa hana kesi ya kujibu na kuachiwa huru.
Matandika
Kaimu Mkurugenzi wa mashindano Martin Chacha Mecky akitoka mahakamani Mara baada ya kuachiwa, kwa kukutwa hapana kesi ya kujibu.
Matandika
Na Karama
Kenyunko
Mahakama ya Hakimu
Mkazi Kisutu imewaachia huru watumishi wawili wa Shirikisho la Mpira wa Miguu
Tanzania (TFF), Martin Chacha na Juma Matandiko baada ya kuwaona hawana
kesi ya kujibu
Uamuzi huo umetolewa
leo na Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi.
Akisoma uamuzi huo,
Hakimu Shahidi amesema kuwa amewaachia huru washtakiwa baada ya kupitia
ushahidi uliotolewa na mashahidi saba wa upande wa mashtaka na kuona upande wa
mashtaka umeshindwa kuthibitisha pasipo kuacha shaka kuwa washtakiwa wametenda
kosa.
Washtakiwa Matandika
na Mecky wanatuhumiwa kwa kuomba rushwa ya Shilingi milioni 25.
Awali ilidaiwa kuwa
Februari 4 mwaka jana, washtakiwa hao wakiwa wajajiriwa wa TFF walishawishi kuomba
rushwa ya kiasi hicho cha pesa kutoka kwa Salum Kulunge na Constatine Morandi
ambao ni maofisa kutoka Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Geita na Klabu ya
Mpira wa Miguu Geita.
Ilidaiwa kuwa watuhumiwa
hao waliomba rushwa hiyo kama kishawishi kwa TFF na Idara ya Uhamiaji Tanzania
kutoa uamuzi dhidi ya klabu ya Mpira wa Miguu Polisi Tabora ili kuisaidia klabu
ya ya Geita kupanda katika ligi kuu ya Tanzania.
Akitoa uamuzi huo,
Hakimu Shahidi alisema katika ushahidi uliotolewa na mashahidi wa upande wa
mashtaka unaonesha hakuna mtu aliyeenda Takukuru kulalamika juu ya washtakiwa
kuomba rushwa zaidi ya sauti ya CD kusambaa katika mitandao.
Amesema upande wa
mashtaka haukuonesha kama kweli washtakiwa walitoka Geita kuja Dar Saalam.
Kuhusu sauti
zilizotambuliwa za Mecky na Matandiko kupitia CD, Hakimu Shaidi amesema watu
wana sauti za kufanana na hata kuigizana hivyo hauwezi kujikita kwenye ushauli
kuwa ni washtakiwa wenyewe ndio wanaosikika kwenye hiyo CD.
Amesema, ni wajibu wa
upande wa mashtaka kuthibitisha pasipo kuacha mashakama kuwa washtakiwa
walitenda kosa hilo.
Hakimu Shahidi ameenda
mbali na kueleza kuwa kwa mujibu wa ushahidi ulitolewa mahakamani hapo,
imedaiwa kuwa kanuni za TFF zinaeleza wazi kuwa, mchezaji akibainika kudanganya
ndiye anayepaswa kuadhibiwa lakini si timu kunyang'anywa pointi.
"Hawa hawakuwa na
mamlaka ya kunyang'anya pointi, hivyo wasingeshtakiwa kwa kuomba rushwa na hata
kama walitenda kosa basi wangeshtakiwa na tuhuma zingine, labda utapeli",
amesema.
Kutokana na upungufu
wa ushahidi, Hakimu Shaidi aliwaachia huru washtakiwa kwa sababu hawana kesi ya
kujibu.
Kesi hiyo ilikuwa
inaendeshwa na Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na
Rushwa (Takukuru),Leonard Swai.
Kaimu Mkurugenzi wa mashindano Martin Chacha Mecky akitoka mahakamani Mara baada ya kuachiwa, kwa kukutwa hapana kesi ya kujibu.