Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala na Diwani wa Vingunguti , Omary Kumbilamoto akizungumza na wazazi wa mtaa miembeni katika kikao cha kamati ya shule.
Baadhi ya Wananchi na Wazazi wakiwa wamekaa kwa makini wakimsikiliza Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala
Mwalimu mkuu wa shule ya Msingi Miembeni,Idaya Ndevumbili akizungumza na wazazi wa shiule hiyo
Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala Omary Kumbilamoto akikabidhi makopo ya rangikwa kamati ya shule ya msingi miembeni
Baadhi ya Wananchi na Wazazi wakiwa wamekaa kwa makini wakimsikiliza Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala
Mwalimu mkuu wa shule ya Msingi Miembeni,Idaya Ndevumbili akizungumza na wazazi wa shiule hiyo
Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala Omary Kumbilamoto akikabidhi makopo ya rangikwa kamati ya shule ya msingi miembeni
Na Humphrey
Shao, Globu ya jamii
Naibu Meya
wa Manispaa ya Ilala, Omary Kumbilamoto amewataka wazazi kuunga mkono juhudi za
Rais Magufuli kwa kuchangia maendeleo ya elimu.
Kumbilamoto
amesema hayo katika mkutano wake na wazazi wa shule msingi miembeni kata ya
Vingunguti .
“lazima
niwambie ukweli hili swala la elimu bure limetusaidia sana katika kata yetu ya
vingunguti hivyo ni vyema kila mtu akawa na wajibu wa kuchangia angalau kidogo
katika maendeleo ya elimu kama sadaka hili watoto wetu waishi katika mazingira
mazuri” amesema Kumbilmoto.
Kumbilamoto
ametolea uwepo wa mabembea katika shule za msingi katika nchi za falme za
kiarabu amabapo alikuwa mapumzikoni hivi karibuni hivyo anasema shule za
vingunguti lazima ziwe na bembea kama za uarabuni.
Aidha amepata
kuchangia ndoo mbili za rangi na makopo manne kwa ajili ya kupakwa katika
darasa la kwanza .
Kwa upande
wake mwalimu mkuu wa shule hiyo Idaya Ndevu mbili alimshukuru Meya huyo kwa
msaada wake na kumuomba aendelee na moyo huo huo