Harusi ya John Focus na Bi. Bernadetha Munishi ilivyofana


Bwana harusi, John Focus Lyimo akimlisha ndafu mkewe kwenye hafla ya harusi yao iliyofanyika Ukumbi wa 'Mwenge Social Hall' jana jijini Dar es Salaam. Harusi yao ilifungwa katika Kanisa Katoliki la Mt. Rita wa Kashia, Kimara Temboni kabla ya hafla hiyo.

Bi. Harusi Bernadetha Francis Munishi (kulia) akimlisha keki mumewe John Focus Lyimo kwenye hafla kabambe ya harusi yao iliyofanyika Ukumbi wa 'Mwenge Social Hall' jana jijini Dar es Salaam. Harusi yao ilifungwa katika Kanisa Katoliki la Mt. Rita wa Kashia, Kimara Temboni.

Bwana harusi, John Focus Lyimo (katikati) akiandaa ndafu maalum kwa ajili ya kumlisha mkewe ikiwa ni ishara ya kumkaribisha nyumbani mara baada ya ndoa yao. Maharusi, John Focus Lyimo na mkewe Bi. Bernadetha Munishi pamoja na wapambe wao wakiwa kwenye hafla hiyo.

Bwana harusi, John Focus Lyimo (wa pili kushoto) akimtambulisha mkewe Bi. Bernadetha Munishi (wa pili kulia) kwa wageni waalikwa kwenye hafla kabambe ya harusi yao iliyofanyika Ukumbi wa 'Mwenge Social Hall' jana jijini Dar es Salaam. Waliokaa ni wapambe wa maharusi.

Dada na mashemeji wa bwana harusi...

Bwana harusi, John Focus Lyimo (kushoto) akipita meza hadi meza kuwashukuru ndugu, jamaa na marafiki walioshiriki hafla kabambe ya harusi yao iliyofanyika Ukumbi wa 'Mwenge Social Hall' jana jijini Dar es Salaam.

Bi. Harusi Bernadetha Francis Munishi (kulia) akipita meza kwa meza kuwashukuru ndugu, jamaa na marafiki walioshiriki hafla kabambe ya harusi yao iliyofanyika Ukumbi wa 'Mwenge Social Hall' jana jijini Dar es Salaam.

Maharusi wakiwaongoza wageni waalikwa kwenye maakuli...

Wanajumuiya wenzake na bwana harusi, John Focus Lyimo kutoka Temboni wakiongozwa na Mr&Mrs Msafiri wakishiriki katika hafla hiyo.

Kulia ni MC Leopold Sondoka (mwenye kipaza sauti) akitoa maelekezo kwa Maharusi, John Focus Lyimo na mkewe Bi. Bernadetha Munishi kwenye hafla hiyo.

Wazazi wa Bwana harusi wakiongozwa na mwakilisha wa Baba ndg, Pius Elias (kushoto) wakizungumza machache kwenye hafla hiyo.

Wazazi na ndugu wa bibi harusi wakipata picha ya ukumbusho.

Familia ya bwana harusi ikiongozwa na mwakilisha wa baba ndugu, Pius Elias wakigonganisha glasi kwa furaha

Meza ya wazazi wa bibi harusi Bi. Harusi Bernadetha Francis Munishi wakionesha furaha yao kwa kugonga chiaz...

Baadhi ya wanakamati ya maandalizi ya harusi hiyo wakigonga chiaz kwa furaha kubwa baada ya kufanikisha shughuli hiyo. Kutoka kushoto ni Mrs. Machonchoryo na Mrs Oscar Munishi.

Maharusi, John Focus Lyimo na mkewe Bi. Bernadetha Munishi wakiwalisha vipande vya ndafu 'mades' wao kama ishara ya kuwashukuru.

Wanakamati wakinyanyua keki waliopewa na maharusi kama shukrani kwa kujitoa na kufanikisha hafla hiyo...

Maharusi, John Focus Lyimo na mkewe Bi. Bernadetha Munishi (kushoto) wakimkabidhi keki ya asante Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi, Bw. Oscar Munishi (kulia).

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi, Bw. Oscar Munishi (kulia) akiwatambulisha wajumbe mbalimbali wa kamati yake.

Meza ya wazazi wa bibi harusi Bi. Harusi Bernadetha Francis Munishi

Post a Comment

Previous Post Next Post