Tembo
zaidi ya 20 wamevamia vijiji vya Wenje mpakani mwa Tanzania na Msumbiji
wakitokea nchini Msumbiji ambapo tembo wawili wameuawa na wananchi na
kuondolewa meno mawili na kugawana nyama yao huku tembo wengine zaidi ya
30 wakivamia kijiji cha jakika wakitokea Pori la Akiba la Selou na
kuharibu zaidi ya ekari 50 za mazao mbalimbali.
Hayo
yameelezwa na Kaimu Afisa wanyamapori wa wilaya ya Tunduru Bw.Limbega
Hassan aliyeongoza kikosi cha askari wanyamapori waliokuwa wakiangalia
usalama wa tembo na wananchi ambapo wananchi wamemng’oa meno mawili
tembo mmoja na kuondoka nayo huku meno mawili ya tembo mwingine
yakisalimishwa kituo cha polisi cha Tunduru.
Kaimu
Afisa wanyamapori huyo wa wilaya ya Tunduru anasema kuwa wamewakamata
watu watano wanaodaiwa kuhusika na kuwaua tembo wawili na kutoweka na
meno huku wekiwatafuta wengine wawili wawachukulie hatua na pia
mikakati ikiwekwa kuwadhibiti tembo katika vijiji vitano
vinavyosumbuliwa na tembo.
Hata
hivyo pamoja na makundi makubwa ya tembo kuingia kwenye vijiji na
kuleta taharuki mkuu wa wilaya Tunduru Bw. Juma Homera amesema kuwa
hali ya usalama iko shwari askari wanyamapori wamefanikiwa kuwadhibiti
tembo hao na hakuna mwananchi aliyedhurika.
CHANZO: ITV TANZANIA
CHANZO: ITV TANZANIA