Kamati ya Viongozi wa dini ya Masuala ya haki za Binadamu ,Kiuchumi na uadilifu katika Uumbaji wakizindua Mapitio ya Ripoti ya Swali la Dola Bilioni moja ,Tanzania inaendelea kupoteza fedha kiasi gani? wakizindua Ripoti hiyo, wakiwa na Wabunge
Kamati ya Viongozi wa dini ya Masuala ya haki za Binadamu ,Kiuchumi na uadilifu katika Uumbaji wakizindua Mapitio ya Ripoti ya Swali la Dola Bilioni moja ,Tanzania inaendelea kupoteza fedha kiasi gani? wakiwa na wabunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakionyesha Vitabu juu mara baada ya uzinduzi
Profesa ,Honest Ngowi akifafanua juu ya Mapitio ya Ripoti ya Swali la Dola Bilioni moja ,Tanzania inaendelea kupoteza fedha kiasi gani?
Askofu Stephene Munga akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mapitio ya Ripoti ya Swali la Dola Bilioni moja ,Tanzania inaendelea kupoteza fedha kiasi gani?
Mbunge wa Msalala , Ezekiel Maige akizungumza wakati wa kuchangia mapitio ya ripoti hiyo
Mbunge wa jimbo la Mufindi kusini Mendrad Kigola akichangia mada
Sehemu ya washiriki wa mkutano huo
Kamati ya Viongozi wa dini ya Masuala ya haki za Binadamu ,Kiuchumi na uadilifu katika Uumbaji wakizindua Mapitio ya Ripoti ya Swali la Dola Bilioni moja ,Tanzania inaendelea kupoteza fedha kiasi gani? wakiwa na wabunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakionyesha Vitabu juu mara baada ya uzinduzi
Profesa ,Honest Ngowi akifafanua juu ya Mapitio ya Ripoti ya Swali la Dola Bilioni moja ,Tanzania inaendelea kupoteza fedha kiasi gani?
Askofu Stephene Munga akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mapitio ya Ripoti ya Swali la Dola Bilioni moja ,Tanzania inaendelea kupoteza fedha kiasi gani?
Mbunge wa Msalala , Ezekiel Maige akizungumza wakati wa kuchangia mapitio ya ripoti hiyo
Mbunge wa jimbo la Mufindi kusini Mendrad Kigola akichangia mada
Sehemu ya washiriki wa mkutano huo
Na Humphrey
Shao, Globu ya Jamii Dodoma
Tafiti mpya iliyozinduliwa leo inasema serikali
inapoteza fedha zaidi ya Sh trillion 4 kwa mwaka kutokana na misamaha na
ukwepaji wa kodi.
Pia repoti inasema serikali inasema serikali
inapoteza Dola za kimarekani 1.3 biloni
(2.9 trilion) kutokana na rushwa na ufisadi katika bajeti ya Taifa.
Hayo
yamesemwa na Profesa Honest Ngowi
alipokuwa akiwasilisha matokeo ya utafiti na mapitio ya ripoti ya swali la dola
bilioni moja na kuja na swali Tanzania inapoteza kiasi gani cha fedha?.
Profesa
Ngowi katika mapitio hayo amepata kutaja kuwa , Mfumo wa ulipaji kodi , Mlipa
kodi,Misamaha ya kodi ,Utroshwaji wa fedha nje ya nchi na upotevu wa mapato,Ukwepaji
kodi, Madhara na Gharama za upotevu na kutokusanywa kodi ipasavyo ni moja ya
mambo yanayochangia kupotea kwa fedha hii.
“Tatizo la
utoroshwaji wa fedha nje ya nchi na upotevu wa mapato limeangaliwa upya katika
utafiti huu na kubaini kuwa Tanzania bado inapoteza mapato kwa njia ya
utoroshaji fedha zilizopatikana kwa njia zisizo halali ,Zinaondoshwa nchini
visivyo na kutumiwa isivyo halali” amesema Prof Ngowi.
Ametaja kuwa
fedha hizo zinaweza kuwa ni fedha zitokanazo na biashara haramu kama biashara
ya kulevya , biashara haramu mipakani ,uharamia ,usafirishaji binadamu ,mapato
kutokana na ukwepaji kodi na mapato yatokanayo na rushwa.
Amesema kuwa sambamba na utoroshwaji wa fedha ,tatizo
la kutoa taharifa za uongo wa bei