Na
Humphrey Shao, Globu ya Jamii
Kaimu Katibu mkuu wa Umoja waa Vijana wa Chama caMapinduzi(UVCMM), Shaka
Hamdu Shaka (MNEC) amesema Umoja wa Vijana
wa Chama Cha Mapinduzi unampongeza Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania kwa na uzalendo wa hali ya
juu alionao kwa Taifa mara baada ya kuchukua maamuzi yenye masalhi ya nchi katika
swala zima la Makinikia.
Shaka amesema hayo leo
mapema jijini Dar es Salaam alipokuwa akitoa tamko la UVCCM kuunga mkono juhudi
za Rais John Pombe Magufuli katika kupambana ma utoroshwaji wa rasilimali za nchi
kwa uzembe wa watanzania wachache.
Amesema Umoja wa Vijana wa CCM unaunga mkono maamuzi yote
yaliyopitishwa au kutolewa na Rais Dk John Magufuli mara baada ya kupokea
ripoti ya Tume ya Uchunguzi
“Umoja wa Vijana wa CCM hatuko tayari na hatutakubali
kushuhudia tena Tanzania ikirejea katika zama ya kiza kinene cha
ukwapuaji mali, ulaji, kufilisi mashirika ya umma au wizi wa mali za
umma.tunaishauri serikali yetu iendelee na mikakati yake ya kuhakikisha
ukwapuaji, ubabaishaji, wizi na ufisadi wa mali za serikali vinavikomeshwa mara
moja
Amesema kuwa Umoja wa Vijana wa CCM unaiomba
kwa dhati Serikali yetu ianze kuipitia upya mikataba yote ya madini ili kubaini
kama ni yenye manufaa na maslahi mapana kwa umma na kumuomba Rais Dk John
Magufuli kuwaweka pembeni wasaidizi wake wote ambao bado wanaonekana kuwa na
kigugumizi katika kuwatumikia wananchi huku baadhi yao wakiona muhali kupambana
na ufisadi.
Ameweka wazi kuwa UVCCM Inasisitiza
kuwa Watendaji wote waliokuwa na dhamana na ambao wamehusika kwa namna moja au
nyingine kupoteza mapato na kulitia hasara Taifa, hatua za kisheria zichukuliwe
dhidi yao haraka .
Amesema wao wanaishauri Serikali kuendelea kuwabaini na
kuwachukulia hatua Viongozi na watendaji wa serikali ambao watabainika kumiliki
mali, utajiri na vitega uchumi ambavyo havitokani na mapato yasiolingana na
vipato vyao wataifishwe kama ilivyofanyika mwaka 1967 baada ya kutangazwa
Azimio la Arusha .
“Vijana wote tunaishauri serikali yetu isikubali na isiafiki
mali za umma zitumike kwa maslahi binafsi badala yake kila miliki ya
serikali na mali ya umma ifahamike kuwa kila mwananchi ana haki kufaidika
nayo ambayo ni sehemu ya matunda ya Uhuru na Mapinduzi matukufu ya Zanzibar”.
Alimaliza kwa kusema kuwa Umoja wa Vijana wa CCM unawataka wana CCM na
Watanzania wote kwa ujumla kuendelea kumuunga mkono Mheshimiwa Rais na Serikali
yake katika mapambano dhidi ya vikundi vya rushwa, ufisadi na uzembe kwa baadhi
ya watendaji ili kuleta maendeleo
endelevu katika taifa letu.
Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Shaka Hamdu Shaka (MNEC) Akiwa amebebwa juu na Vijana wa CCM
Sehemu ya Vijana wa Hamasa wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi wakifurahi juu ya mamuzi yaliyochukuliwa na Rais John Pombe Mgufuli
Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Shaka Hamdu Shaka (MNEC) akiwasili katika ukumbi wa Umoja wa Vijana KinondoniKaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Shaka Hamdu Shaka (MNEC) akiwasili katika Ukumbi wa Umoja wa Vijana Kinondoni
smsehemu ya Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wakiwa na furaha kubwa sana
ehemu ya Vijana wa Hamasa wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi wakifurahi juu ya mamuzi yaliyochukuliwa na Rais John Pombe Mgufuli
Mabango ya kumpongeza Rais Magufuli