HOSPITALI YA AGA KHAN YAZINDUA HUDUMA MPYA YA GHARAMA NAFUU

Mtoto wa Aga Khan Princes Zahra Aga Khan azindua huduma mpya ya huduma za gharama na fuu kwa wagonjwa na Maabara ya kisasa  katika Hospitali ya Aga Khan jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Meneja mawasiliano wa Hospitali hiyo Olayce Lotha amesema kuwa maabara hiyo itasaidia kutoa majibu ya vipimo ambavyo vililazimika kupelekwa nje na kurudi hili waendelee na matibabu.

“tumetengeneza mfano wa vitanda 20 ambavyo vitaonekana katika mradi huu, pia kwa sasa maabara hii mpya itaweza kutoa majibu yote ya vipimo vya kansa na magonjwa mengine sugu ambayo yalikuwa lazima yakapimwe nje ya nchi” amesema Lotha.

Amesema wodi hizo kwa sasa zitaweza kuchukua watu wanne kwa pamoja kwa gharama nafuu tofauti na zile wodi zingine ambazo zilikuwa zinachukua mtu mmoja mmoja kwa gharama ya hali ya juu.

Amesema mradi huo umetokana fedha kutoka Msaada kutoka kwa Tasisi ya Maendeleo ya ufaransa (FDA) ambayo imetoa Bilioni 120 na bilioni  60 kutoka Aga Khan Development Network.


   

Post a Comment

Previous Post Next Post