Na Humphrey
Shao, Globu ya Jamii
Mamlaka ya
kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya imekamata kontena mbili zilizobeba
kemikali bashirifu zilizokuwa tayari kwa kuingizwa nchini katika eneo la
bandari kavu ya Ami Tabata Relini.
Zoezi hilo
la ukamataji huo ambalo liliongozwa na kamishna Mamlaka ya kupambana na Kudhibiti dawa hizo Siang’a
akiwa ameongoza na maofisa wa nagazi za
juu.
Akizungumza wakati
wa zoezi la ukaguzi wa kemikali hizo Kamishna Msaidiz wa ukaguzi wa kemikali
jinai , Mamuya amesema kuwa mzigo huo ni mwendelezo wa mzigo wa kampuni ya
Tecno Scientific ambayo ilikuwa ikifanyia shughuli zake katika eneo la Mwenge
jijini Dar es Salaam
Amesema hapo
awali waliweza kukamata lita 10,000 na mzigo ulikouwa umeingizwa katika bandari
ya Dar es Salaam ulikuwa lita zaidi ya 6000 zikitokea nchini ufaransa.
Ametaja kuwa
mamlaka inaendelea na uchunguzi wa kuzichunguza kemikali hizo hili kubaini kama
zimefuata njia sahii ya kuingia nchini .
Amesema kuwa
ikibainika kuwakemikali hizo zimeingia kinyume cha sheria wanao husika
watapelekwa mahakamani.
Baadhi ya watendaji wa Mamlaka ya Udhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), wakikagua kemikali ziliozpo ndani ya maboksi na kuchukua sample
mzigo wa kaemkali bashirifu ukipakuliwa ndani ya kontena katika eneo la bandari kavu ya Ami tabata jijini Dar es Salaam
Kamishna Msaidzi wa ukaguzi kemikali jinai wa Mamlaka ya Udhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya akiweka alama maboksi yaliyokutwa na kemikali bashirifu
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Rogers Siang'a akiangalia mzigo wa kemikali bashirifu
Mmiliki wa Kiwanda cha Tecno Scientific akiwa amekaa katika eneo la bandari kavu akiangalia mzigo wake unavyokaguliwa
wafanyakazi wa TRA na Mamlaka ya Udhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), wakikagua siri za kufungia kontena hili waweze kulifungua