PBZ YAWAKARIBISHA WADAU KUFUNGUA AKAUNTI KATIKA BANDA LAKE LA MAONESHO LA SABASABA

 Afisa Teknohama wa Islamic Benki ya PBZ ,Rahma Ali akizungumza na mmoja wateja waliofika katika banda lao la Maonyesho lililopo katika Viwanja vya Maonyesho ya Sabasaba  ambapo benki hiyo inawezesha kufungua akaunti ya Islamic benki na kuwezesha kupata mkopo usiokuwa na riba.
 Afisa Mahusiano wa PBZ -Bank LTD ,Aisha  Ali Mohd akizungumza na mmoja wa wadau waliofika katika banda la PBZ kupata maelekezo namna ya kufungua Akaunti kwenye benki hiyo


 Afisa  Masoko  PBZ Bank, Anas  Rashid Ramadhani akizungumza na wateja juu ya huduma za mikopo na ufungaji wa akaunti katika benki hiyo pamoja na ununuzi wa Viwanja kwa njia ya mkopo ambao utalipwa ndani ya miaka 10 wakati wa Maonyesho ya Sabasaba
 Wafanyakazi wa PBZ ,Hamyer Said na Biubwe Vuai wakimuelekeza mteja aliyefika katika banda hilo faida za Islamic Bank
 Salehe Abdalah akizungumza na mmoja wa wateja waliofika katika banda la Benki ya watu wa Zanzibar PBZ kutaka kufungua akaunti wkati wa Maonesho ya Sabasaba


Mwajuma Njaritu wa PBZ Islamic Bank akizungumza na mteja faida za huduma hiyo kwa waislamu

Post a Comment

Previous Post Next Post