Diwani
Kata ya Msigani, Ubungo, Israel Mushi ( 48 ) na Mrasimu ramani wa Manispaa ya
Ubungo, Francis Mwanjela Peter ( 28 ) wamekamatwa na Tasisi ya kuzia na kupambana na Rushwa nchini 'TAKUKURU' Mkoa wa Kinondoni
kwa tuhuma za kuomba na kupokea rushwa Sh.5,000,000/=.
kwa mujibu wa taharifa iliyotolewa na Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Kinondoni Teddy Mjangira amesema kuwa Watuhumiwa
walikamatwa Julai 12, 2017 baada ya kupokea kiasi hicho cha pesa toka kwa
mwananchi ambaye jina lake limehifadhiwa na ambaye mbali na kutoa kiasi hicho
cha pesa alitakiwa na watuhumiwa kuwapa rushwa ya Sh.10,000,000/=
Watuhumiwa
walishawishi na kupokea rushwa ili waweze kutoa ushawishi kwa wajumbe wa kamati
ya mipango miji inashughulikia maombi ya
kubadilisha michoro, kubadilisha matumizi ya kiwanja na kupitisha kibali cha
ujenzi katika Manispaa ya Ubungo.
Uchunguzi
wa tuhuma unaendelea na Watuhumiwa ambao wanatuhumiwa kutenda makosa kinyume na
kifungu namba 15 cha sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Namba 11 ya mwaka
2007 wamepewa dhamana.
Mkuu
wa TAKUKURU (M) Kinondoni Bi.T. MNJAGIRA anawaasa Viongozi wote wa Umma,
Wanasiasa na Watumishi wote wa Serikali, kuheshimu nyadhifa zao na kutekeleza
majukumu yao kwa kuzingatia sheria bila kujihusisha na vitendo vya Rushwa. Pia,
anatoa wito kwa Wananchi wote kuendelea
kutoa ushirikiano kwa TAKUKURU kwa kuwafichua wale wote wanaojihusisha na vitendo vya rushwa ili waweze kuchukuliwa
hatua za kisheria, Kwa kufanya hivyo, tutakuwa tumezuia vitendo hivyo
visiendelee kujitokeza katika Jamii