Na Humphrey
Shao, Globu ya Jamii
Waziri wa
Madini , Angela Kairuki amesema kuwa serikali inataraji kupata mrabaha Zaidi katika
madini ya Almasi yaliyokamatwa katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu
Julius K Nyerere kutoka kwa Kampuni ya Williamson Diamond iliyokuwa ikikitaka kutoroshwa nchini kwenda
nchini Ubelgiji.
Waziri
kairuki amesema hayo alipokuwa akizungumza na Waandishi wa habari wakati akitoa
ripoti ya Wizara ya Madini juu ya mzigo huo wa Almasi kutoka kampuni ya
Williamson Diamonds.
“tarehe
20/10/2017 almasi hizo zilisafirishwa kwenda ubelgiji na serikali ilituma
maafisa wake kusimamia uuzwaji wa alamasi hizo ambapo tarehe 7/11/2017 almasi
hizo ziliuzwa kwa dola za Marekani 10,261,227.76 hivyo thamani hii ni ongezeko
la Dola za Marekani 2,069,582.77 sawa na asilimia 20.16%”amesema.
Amesema kutokana
na ongezeko hilo baada ya almas kuuzwa serikali itapata mrabaha Zaidi ambao ni
mwisho kiasi cha Dola za Marekani 124,174,.97 na ada ya ukaguzi Dola za
marekani 20,695.83 ambayo jumla yake ni dola za Marekani 144,870.80 sawa na
shilingi Milioni 325.525 hivyo jumla ya mapato yote ya serikali kutokana na
mauzo ya almasi hizi ni Dola za Marekani 718,288.95
Aidha waziri
kairuki amesema katika mzigo huo waliweza kuikuta Almasi moja yenye rangi ya
pinki ambayo ni adimu kupatikana na yenye uzito wa karatani 5.92 na kuuzwa kwa
dola za marekani 2,005,555.00 sawa na shilingi Bilioni 4.51 .
Alimaliza kwa
kusema kuwa anawakikishia Watanzania kuwa serikali itaendelea kuismamia kwa
umakini rasilimali zetu za madini ili kuhakikisha kuwa nchi yetu inanufaika
ipasavyo.
Waziri wa Madini Angela Kairuki akizungumza na Waandishi wa Habari juu ya ripoti ya faida iliyopata serikali katika Madini ya Almas kutoka mgodi wa Wiliamson Diamonds Ltd iliyokamatwa uwanja wa ndege wa Jk Nyerere.Waziri wa Madini Angela Kairuki akizungumza na Waandishi wa Habari juu ya ripoti ya faida iliyopata serikali katika Madini ya Almas kutoka mgodi wa Wiliamson Diamonds Ltd iliyokamatwa uwanja wa ndege wa Jk Nyerere.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini . Prof.Simon Msanjila akitoa ufafanuzi wa kitaalmu juu ya madini hayo yaliyouzwa huko ubelgiji.
Kamishana wa Madini Mhandisi Benjamini Mchwampaka akizungumzia juu ya madini hayo yanavyoweza kuliongezea pato taifa.
Wahariri wa gazeti la Jamhuri Mkinga Mkinga na Deodatusi Balile wakiteta jambo katika mkutano huo