Dar es Salaam, Tanzania Desemba 02, 2017. Kampuni ya michezo ya kubashiri ijulikanayo kama SportPesa Limited
imeidhamini timu ya mpira wa miguu na kikapu ya Bunge la Tanzania ambao
wanatarajia kushiriki mashindano ya wabunge wa Afrika Mashariki mnamno Desemba
3, 2017 katika uwanja wa Taifa, Temeke Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari katika
ofisi za SportPesa zilizopo Masaki, Peninsula House Mkurugenzi
wa Utawala na Utekelezaji SportPesa Tanzania Mr. Tarimba Abbas alisema
“Tulivyosikia kuwa haya mashindano ya wabunge wa Afrika Mashariki kwa mwaka huu
yatafanyika nchini kwetu tuliona ni vyema kuwa wazalendo kwa kuidhamini timu ya
mpira wa miguu na pete kwa kutoa vifaa mbalimbali vya michezo kama Jersey,
bibs, soksi, pamoja na mipira. SportPesa ni kampuni ya kubashiri michezo
mbalimbali ikiwa na kengo kuu la kukuza na kuendeleza sekta ya michezo nchini
na ndiyo maana tulianza kwa kudhamini timu za mpira wa miguu za Simba, Yanga na
Singida United.
“Mbali na hapo
tutatoa tracksuits kwa ajili ya wabunge wote 160 wanaoshiriki katika mashindano
hayo siku ya ufunguzi ambapo wabunge hao watafanya maandamano kutoka ukumbi wa
PTA SABASABA kuelekea Uwanja wa Taifa kwa ajili ya kuanza michezo mbalimbali ya
ufunguzi.”
“Tunapenda
kuwapongeza na kuwatakia kila lakheri timu ya Bunge la Tanzania katika
mashindano haya na tunaamini wataiwakilisha vizuri nchi yetu” alimaliza Mr.
Tarimba
Naye Mwenyekiti
wa klabu ya michezo ya wabunge Mh. William Ngeleja alianza kwa kusema
“tunapenda kutanguliza shukrani zetu za dhati kwa kampuni ya michezo ya
kubashiri SportPesa kwa ushirikiano wao waliouonyesha na kutusapoti katika
kuhakikisha timu zetu za mipira wa miguu na pete zinapata vifaa vya michezo
kama vile jezi, mipira na soksi.
“Tunatarajia
kuanza rasmi mashindano yetu siku ya jumapili tarehe 03, desemba 2017 ambapo
kutakuwa na shughuli mbalimbali za ufunguzi huo ikiwemo kukimbia, kuvuta kamba,
mpira wa pete, mpira wa wavu pamoja ja mpira wa miguu”.
“Michezo hii
itahusisha wabunge kutoka nchi za Afrika Mashariki ikiwemo Tanzania, Kenya,
Uganda na Burundi. Timu zetu za mpira wa miguu na mpira wa pete zitacheza na timu
ya wabunge wanaoiwakilisha nchi ya Burundi siku ya jumatatu tarehe 04 desemba
2017, alimaliza Mh. Ngeleja.
Mashindano haya
yatafunguliwa kwa michezo ya riadha pamoja na kuvuta kamba huku wengine
wakijiandaa na Jumatatu ambapo timu za mpira wa miguu, Pete, pamoja na mpira wa
wavu wakijiandaa kwa siku iliyofuata.
Mashindano ya
mpira wa miguu yanatarajiwa kufanyika katika uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaam ambapo uwanja huu uliofanyiwa marekebisho makubwa na kampuni ya michezo
ya kubashiri SportPesa na kukabidhiwa kesho kabla ya ufunguzi wa mashindano
hayo.