AFRIKA ZINDUKA YA BAGAMOYO PLAYERS YATIKISA KIGODA CHA NYERERE



Na Sophia Mtakasimba(TaSUBa)
Mchezo wa kuigiza wa jukwaani unaofahamika kwa jina la Afrika zinduka, umetikisa tamasha la kumi la kigoda cha Mwalimu Nyerere lililoendelea  katika ukumbi wa Nkuruma wa chuo kikuu cha Dar es Salaam.

Mchezo huo uliobeba ujumbe wa namna  Bara la Afrika linavyoteseka na umasikini mkubwa ile hali  lina utajiri mkubwa wa mali asili , ardhi na madini umetungwa , umeongozwa na kuchezwa na Kikundi cha “Bagamoyo Players” cha Taasisi ya Sanaa na utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) ili kuchagiza ujumbe wa tamasha la mwaka huu uliosema “wimbi la uporaji wa rasilimali Afrika wanyonge wanajikwamuaje”

Akizungumza katika siku ya pili ya Tamasha hilo Mwenyekiti wa Kigoda cha Taaluma cha mwalimu Nyerere, Profesa Penina Mlama , amesema kuwa igizo hilo limeakisi namna halisi ya maisha ya sasa ya muafrika hivyo ni wakati wa kuzinduka.

“Wenzetu wa TaSUBa wametuambia Afrika Zinduka ,sasa huu ndio wakati wetu wa kuzinduka na kuona namna Afrika inaweza kunufaika na rasilimali zake.” Alisema bi Mlama

Tamasha la kigoda cha kitaaluma cha Mwl,nyerere  ambalo kwa mwaka huu limetimiza miaka kumi toka kuanzishwa kwake limefanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 11-13 Aprili  ambapo mada mbalimbali kuhusu masuala ya kijamii zimejadiliwa .
 Wasanii wa kikundi cha Bagamoyo Players cha TaSUBa wakionyesha igizo la Afrika Zinduka katika tamasha la kumi la kigoda cha mwalimu Nyerere.
 Wasanii wa kikundi cha Bagamoyo Players cha TaSUBa wakionyesha igizo la Afrika Zinduka katika tamasha la kumi la kigoda cha mwalimu Nyerere.
Wasanii wa kikundi cha Bagamoyo Players cha TaSUBa wakionyesha igizo la Afrika Zinduka katika tamasha la kumi la kigoda cha mwalimu Nyerere.
washiriki wa tamasha wakifuatilia igizo la Afrika Zinduka

Post a Comment

Previous Post Next Post