Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo amesema wizara yake kupitia wakala wa Barabara wa Serikali za Mitaa Tarura itafanya upembezi wa haraka hili kuwez akuhakikisha miundombinu ya barabara iliyoaribika kutokana na mvua za Masiaka katika barabara za manispaa ya Ilala inarekebishwa haraka sana.
Waziri jafo amesema hayo mapema
leo Jijini Dar es Salaam alipotembelea madaraja mawili yaliyo katika na maji ya
kata ya Gongolamboto Ulongoni A na B na
Pugu Mnadani, ambapo yamesababisha watu kushindwa kuvuka kwa magari kutoka
upande mmoja kwenda mwingine.
“ Hili la ulongoni A
litashughulkikiwa kwa haraka kutokana na laenyewe kuonyesha unafuu kidogo
lakini Darja la ulongoni B na Pugu wataalamu watabidi wakachini hili waweze
kujua ni namna gani yatajengwa hili yasiweze kupata tena madhara pindi mvua
kubwa zinaponyesha”amesema Jafo.
Aidha waziri jafoi aliwaomba wale wote waliojenga katika kingo za mto msimbazi kuanz akuondoka haraka kwani madhgara yake ni makubwa kama yalivyoonekana katika mvua hizi ambapo nyumba nyingi zimesombwa na maji na watua wana pa kukaa.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo akiwa ameongozana na Viongozi waandamizi wa Manispaa ya Ilala kwenda kuanaglia bafrabra na Madaraja yaliyo athirika wakati wa Mvua.W Mkuuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema akimuonesha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo Sehemu ya Miundombinu iliyoharibika
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo akizungumza na Viongozi Waandamizi wa Manispaa ya Ilala waliongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Sophia Mjema wakati alipofanya ziara ya kukagua miundombinu ya barabara za Halmashauri.
Sehemu ya Draraja la Ulongoni A iliyochukuliwa na Maji ambayo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo alikwenda kukagua