SETHI AIBUKA, APINGA KUNG'OLEWA IPTL



Na Mwandishi Wetu

Mkurugenzi na Mmilikiwa kampuni ya PAP/IPTL ,Harbinder Sing Sethi Amekanusha taarifa zinazosambzwa mitandao kuwa amefutwa kuwa Mwenyekiti na Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo.
Hayo yameelezwa leo na Mwanasheria   wa mmiliki wa Kampuni ya PAP/IPTL, Harbinder Sing Sethi, Hajra Mungula, mara baada ya kupokea taarifa kutoka kwa mteja wake na kusema Sethi bado Mwenyekiti na Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo.

Wakili Mungula amesema kuwa   watanzania kupuuza kwa taarifa zilizotolewa awali na watu wanaojiita kuwa Mwenyekiti na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni hiyo.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa  na Wakili  Hajra Mungula imesema kuwa  yeye kama mwanasheria wa Sethi, amewasiliana na mteja wake, ambaye yuko rumande na kushangazwa na taarifa hizo.

Ilisema hivi karibuni kumeripotiwa taarifa kwenye vyombo vya habari kwamba kampuni inayomilikiwa na Harbinder Sing Sethi imebadilisha uongozi katika ngazi za Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi na Mkurugenzi mtendaji wake.

"Taarifa iliyosambazwa na anayejiita mwenyekiti wa bodi mpya, Ambroce Brixio imemtaja yeye kuwa na cheo hicho na Joseph Makandege kuwa Mkurugenzi wake ambaye kwa miezi kadhaa sasa hajawahi kuonana nae ikiwemo hata kutofika mahakamani siku ambazo kesi imekuwa ikitajwa" imesema sehemeu ya taarifa hiyo.

Wakili Hajra, aliandika katika taarifa hiyo kuwa taarifa hizo zimemfikia kwa masikitiko makubwa Mwenyekiti halali na mmiliki wa kampuni hii ya kuzalisha umeme ya IPTL ambayo kimsingi inamilikiwa na kampuni anayoimiliki ya Pan Africa Power Solutions(PAP).

Kwa mujibu wa taarifa ya mwanasheria huyo, pamoja na kuagiza wanasheria wake kuchukua hatua za haraka za kisheria mwenyekiti Sethi pia hana taarifa zozote juu ya mabadiliko hayo.

"Mwenyekiti Seth anapenda kuutaarifu umma kupitia sisi kwamba wazipuuze taarifa hizo kwa kuwa hazitokani na mamlaka halali za kisheria za kampuni hiyo," ilisema mwanasheria huyo.

Ilisema pamoja na kwamba Mwenyekiti Sethi bado yuko mahabusu akituhumiwa mashtaka kadhaa ya jinai, hiyo haiondoi ukweli kuwa IPTL ni kampuni binafsi yenye wamiliki halali wenye hisa halali na wala sio NGO ambayo mtu yeyote anaweza kutangaza mapinduzi ya kiuongozi wakati wowote.

"Mwenyekiti anapenda kuwahakikishia watanzania wote kuwa licha ya uwepo wa mashtaka yanayomkabili bado kampuni hiyo ipo chini ya usimamizi salama wa PAP na kwamba madeni yote, madai, mali na stahiki zote zizohusiana na kampuni hiyo zipo katika mikono salama mpaka sasa" ilisema sehemu ya taarifa

Aidha, ilisema taarifa hiyo, Mwenyekiti anawahakikishia watanzania kuwa ataendelea kutoa ushirikiano mahsusi kuhakikisha nchi inajiepusha na hasara zinazotokana na matendo ya aina ya kina Makandege na wenzake ya kukurupuka bila kufuata sheria na taratibu


Post a Comment

Previous Post Next Post