MAHAKAMA TIDO MHANDO ANAKESI YA KUJIBU KATIKA MASHTAKA YANAYOMKABILI

NA EUNICE SHAO


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo Agosti 27, 2018  imemkuta Mkurugenzi mkuu wa zamani wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Tido Mhando anayekabiliwa na mashtaka ta matumizi mabaya ya madaraka ana kesi ya kujibu.

Uamuzi huo umetolewa na Hakimu Mkazi Mkuu Huruma Shahidi baada ya upande wa mashtaka kufunga kesi yao kwa kuleta mashahidi watano.

Hakimu Shaidi amesema, amepitia ushahidi wote wa mashahidi watano ulioletwa na upande wa mashtaka na kuona mshtakiwa ana kesi ya kujibu.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo Agosti 27, 2018  imemkuta Mkurugenzi mkuu wa zamani wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Tido Mhando anayekabiliwa na mashtaka ta matumizi mabaya ya madaraka ana kesi ya kujibu.

Uamuzi huo umetolewa na Hakimu Mkazi Mkuu Huruma Shahidi baada ya upande wa mashtaka kufunga kesi yao kwa kuleta mashahidi watano.

Katika kesi hiyo Tido anakabiriwa na
mashtaka manne ya kutumia madaraka vibaya na moja la kuisababishia Serikali hasara ya Sh887.1 milioni.

Kabla ya kutolewa kwa uamuzi huo, leo shahidi wa tano wa upande wa mashtaka, Dominic Mahundi alitoa ushahidi wake.

Miongoni mwa  mashahidi  wa upande wa mashtaka waliotoa ushahidi ni ofisa uchunguzi wa Takukuru, Victor Lesuya;  mwanasheria wa TBC, Gwakisa Mlawa na mkurugenzi Mkuu mstaafu wa TBC, Clement Mshana.

Katika kesi hiyo inadaiwa kuwa Juni 16, 2008,  akiwa  Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Tido ambaye alikuwa mkurugenzi wa TBC, kwa makusudi alitumia madaraka yake vibaya kwa kusaini mkataba wa kuendesha na utangazaji wa vipindi vya televisheni kati ya TBC na Channel 2 Group Corporation (BV1) bila ya kupitisha zabuni, kitu ambacho ni kinyume na Sheria ya Manunuzi na kuinufaisha BVl.

Tido  ambay anatetewa na Wakili Ramadhani Maleta na yupo nje kwa dhamana ataanza kujitetea Septemba 20.2018

Katika kesi hiyo Tido anakabiriwa na
mashtaka manne ya kutumia madaraka vibaya na moja la kuisababishia Serikali hasara ya Sh887.1 milioni.

Kabla ya kutolewa kwa uamuzi huo, leo shahidi wa tano wa upande wa mashtaka, Dominic Mahundi alitoa ushahidi wake.

Miongoni mwa  mashahidi  wa upande wa mashtaka waliotoa ushahidi ni, ofisa uchunguzi wa Takukuru, Victor Lesuya;  mwanasheria wa TBC, Gwakisa Mlawa na mkurugenzi Mkuu mstaafu wa TBC, Clement Mshana.

Katika kesi hiyo inadaiwa kuwa Juni 16, 2008,  akiwa  Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Tido ambaye alikuwa mkurugenzi wa TBC, kwa makusudi alitumia madaraka yake vibaya kwa kusaini mkataba wa kuendesha na utangazaji wa vipindi vya televisheni kati ya TBC na Channel 2 Group Corporation (BV1) bila ya kupitisha zabuni, kitu ambacho ni kinyume na Sheria ya Manunuzi na kuinufaisha BV

Post a Comment

Previous Post Next Post