AIBU NYINGINE KWA ZITTO ASHUKIWA NA KUAMBIWA AACHE UONGO

Sehemu ya Mataluma ya Reli yaliyoppo katik autekelezaji w amradi wa ujenzi wa Reli sgr Katika eneo la Soga Mkoani Pwani
Na. HABIB MCHANGE

Ninamfahamu vema sana Zitto Kabwe,  nina hakika kabisa hoja yake aliyoitoa leo kuhusu ujenzi wa reli ni ama hajui anachokisema au anaendelea na utaratibu wake ule ule wa kujifanya anajua kila kitu kuliko mtu yeyote hapa nchini

Kwa muda sasa Zitto amekuwa akipambana kuuaminisha umma kuwa ni yeye tu ndio Mtanzania mwenye akili kuliko mtu yeyote,  mwenye kujua kila kitu kuliko mtu yeyote,  mjanja kuliko kila mtu na ndie mwanasiasa mwenye kujua kuliko mwanasiasa yeyote kiasi cha kuwaona wenzake wote vilaza

Sisi tunaomfahamu Zitto na wenzake hatupati shida kuhangaika kumjibu anaporopoka maneno yake na data zake za kuunga unga

Zitto leo amesema serikali inakwamisha mradi liganga na mchuchuma kwa madai ya kitoto kabisa

Ama Zitto amesahau kuwa amekuwa kiongozi msimamizi wa Rasilimali mwenyekiti wa PAC kwa miaka mingi kuliko Mtanzania yeyote ikiwemo hiyo liganga na mchuchuma na wala hakuna cha maana alichoifanyia migodi hiyo mpaka leo

Pengine pia hajui kuwa serikali hainunui reli, hainunui taruma wala hainunui kitu chochote katika mradi wowote unaoendelea na badala yake manunuzi hufanywa na mkandarasi aliyeshinda zabuni na hivyo ni wajibu wake kuamua anunue nini wapi na kwanini huku serikali kazi yake ikiwa ni kuhakikisha inapatiwa huduma kwa kadri ilivyo kwenye mkataba

Leo Zitto hajui haya au porojo tu kama jana na juzi?.... anataka watanzania tushiriki kugombea tender zinazogombewa na makampuni ya kusambaza na kuuza chuma kweli?

Tumpuuzeni tu aisee na tuendelee kumuunga Mkono Rais Magufuli kwa kazi hii iliyotukuka anayoifanya

Nina hakika Zitto hana ufahamu wa kinachoendelea Site kuhusiana na mradi huu wa SGR.

Nimepita bahati ya kutembelea maendeleo ya mradi mkubwa na wa kihistoria wa ujenzi wa Reli yetu ya kisasa tena ya umeme wa Standard Gauge uliopangwa kujengwa kutoka DAR mpaka Mwanza na baadae kigoma na maeneo mengine ya nchi mradi ambao umewekwa kutekelezwa kwa awamu kadhaa huku awamu ya kwanza ikiwa ni DAR mpaka Morogoro KM 205 za njia kuu ya reli na zaidi KM 95 za mapishano na shughuli nyingine muhimu

Naomba nikiri hadharani,  kabla sijaenda kujionea kinachoendelea Site akili na mtazamo wangu juu ya mradi huu yalikuwa kama Zitto na wengine wanavyowaza.

Sikuwa nikijua kuwa mradi huu umeenda kuzalisha maelfu ya ajira za moja kwa moja kwa vijana na watu wa rika nyingine hapa nchini.

Sikuwa nikijua kuwa mradi huu umeongeza kwa kiasi kikubwa sana mnyororo wa kiuchumi

Nimeshuhudia kwa macho yangu tena zaidi ya mara moja namna vijana wa kitanzania wakitengeneza Mataruma yanayotumika kujengea reli hii muhimu ya kihistoria

Nimeona kwa macho yangu vijana wa kitanzania wakipata ujuzi wa kukunja nondo kitaalam zinazotumika katika maeneo mbalimbali ya ujenzi

Nimeona kwa macho yangu namna ambavyo mradi huu umeongeza kwa kiasi kikubwa sana uhaba wa saruji hapa nchini kutokana na uhitaji mkubwa wa bidhaa hiyo katika ujenzi wa mataruma,  madaraja, nguzo na  majengo mengine.

Mradi huu umenionyesha kwa sababu gani Nondo zimepanda bei mtaani kutokana na uhitaji wake mkubwa kwenye ujenzi wa mradi,

Kwa kifupi kabisa,kama Mtanzania nimefurahi sana kuona mradi unatumia malighafi na bidhaa zilizotengenezwa ndani kwa zaidi ya asilimia 50 ya mahitaji yake

Zaidi nimefurahi kuona Mataruma yanayotandikwa katika reli hii yanatengenezwa Tanzania katika kiwanda cha mataruma kilichopo Soga na baadae kiwanda kingine kitakamilika katika site ya Kilosa

Kifupi tu niseme,  kama kuna kitu Magufuli amewahi kukifanya na ataendelea kukumbukwa leo akiwa hai na kesho asipokuwepo basi ni uamuzi huu wa kiume wa ujenzi wa reli hii ya kisasa.

Magufuli ameendelea kutupa heshima sio tu watanzani lakini waafrika kwa ujumla wake kwa uthabiti na ushujaa huu.

Achana na habari ya mafanikio yake ya kihistoria katika sekta mbalimbali hapa nchini ikiwemo Afya, Elimu Bure, mapambano dhidi ya Rushwa, Ujenzi wa Miundombinu, ununuzi wa ndege na kadharika,  Hii ya Standard Gauge ni Heshima itakayodumu vizazi na vizazi.

Tumesoma shule ya msingi na baadae sekondari kuwa reli maarufu nchini inayoanzia Dar mpaka Kigoma ikipita pia mwanza kutokea Tabora (Reli ya Kati) ilianza kujengwa na wakoloni wa kijerumani  kati ya miaka 1905 na kuendelea.

Leo JPM ameamua kufuta historia hiyo ya wakoloni na kuandika historia mpya.  Naam historia mpya hii inaandikwa kwa kutumia fedha za ndani tena bila hofu wala wasiwasi wowote

Magufuli ametufanya tutembee kifua mbele.

Ukianza safari pale stesheni ukaona jinsi watu wanavyopiga kazi,  vyuma vikigongana,  magari yaliyobeba materials yakiwajibika utaelewa nini ninachokisema

Ukisogea shauri moyo ilala ukashuhudia ujenzi wa daraja la juu la zaidi ya Kilomita mbili na nusu litakalobadilisha pia mwonekano wa jiji la DAR,

Ukaambaa ambaa na reli ukafika Pugu na kushuhudia ujenzi wa stesheni ya kisasa ya eneo hilo lililo kilomita 20 kutoka stesheni hakika utasema Magufuli ANATENDA

Akitoka pugu akaambaa ambaa na njia ya mkandarasi inayojenga reli hiyo kuelekea soga,  njiani utajionea mwenyewe namna miamba ilivyopasuliwa, milima imechongwa tuta limewekwa kwa ustadi nakuhakikishia hautatamani kuacha kumpongeza JPM

ukifika Soga ukaona kambi ya ujenzi wa reli hiyo,  ukaona namna mataruma yanavyotengenezwa, ukaona reli iliyotandazwa juu ya tuta na ukasogea pembeni ukaona nyasi za kisasa zilizooteshwa kudhibiti uharibifu wa mazingira hauwezi kuelewa wala kusikiliza POROJO ZA ZITTO na wenzake

Ukisogea mbele ya soga kuelekea Ruvu,  ukakutana na Daraja kubwa la upana wa mita 11 na upana wa zaidi ya mita 6 linalotenganisha barabara na treni huku treni ikipita juu barabara chini,  nakuambia Zitto na wenzake wote wa aina yake lazima uwapuuze kama sio kuwadharau kabisa

Hebu sogea Ruvu basi kidogo,  nenda kajionee namna maji yalivyofinyangwa finyangwa kuweka njia ili mitambo ipite wewe,  Zitto huwezi muamini tena

Sogea basi Kwala pale,  ujionee eneo kubwa linalojengwa Marshalling Yard eneo ambalo zaidi ya treni yenye urefu wa kilomita mbili zinaunganishwa na kupishana huku pembeni kidogo pakiwa na bandari kavu, halafu Zitto na wenzake wanaleta hadithi za Arifu lela olela?

Toka Kwala sasa sogea mpaka Ngerengere uone shughuli nyingine zinazoendelea, njoo mpaka Moro mjini ujionee mitambo inavyofanya kazi halafu usikilize takataka za kina zitto hizi, utatamani kutema mate chini.

Toka Moro elekea Dodoma kupitia Kilosa na GULWE, angalia namna ambavyo wanaume wanachoronga milima ya kilosa ili kupitisha Treni mita 90 Ardhini,  halafu wahuni wachache wanasemaje?

Njoo mpwapwa uone namna vijana wanavyopiga kazi mchana na usiku kuelekea Ihumwa.  Weweeee? Acheni tu jamani

Hapo sijakueleza kuhusu idadi ya  ajira zilizozalishwa, unaambiwa zaidi ya watanzania 5900 wameajiriwa kufanya ujenzi wa mradi huu utakaodumu na kudumu katika akili za watanzania

Sijakwambia kuhusu madaraja, njia za juu, njia za chini, vivuko,  majengo ya stesheni na mambo mengine.

Sijakwambia pia juu ya namna elimu inavyopandikizwa kwa wazawa wanaoshuhudia ujenzi wa mambo mbalimbali kutoka kwa wataalam wa kimataifa.

Kuendelea kuwasikiliza wapotoshaji wa aina ya Zitto ambao wao kila kitu wanataka kufanya siasa ama kiki ni kujipotezea muda tu. Standard Gauge inajengwa kwa kasi ya ajabu na mwaka 2020 Zitto na wenzake watasafiri na reli hiyo hiyo wanayoionea donge

Ndimi tena
Habib Mchange
0762178678
Morogoro, Tanzania

Post a Comment

Previous Post Next Post